Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2017

UHUSIANO KATI YA UGUMBA NA UPUNGUFU WA MADINI YA ZINC

  Zinc ni elementi muhimu mno katika afya ya binadamu hivi kwamba ukosefu kidogo unaweza kuleta madhara makubwa. Zinc ni ya muhimu sana kwa sababu inapatikana ndani ya kila kiungo cha mwili cha binadmu na inahusika kwa karibu sana na kugawanyika kwa seli za mwili. Ni antioxidant yenye nguvu sana, inayosaidia kuzuia kansa, na pia inahusika moja kwa moja katika ufanyaji kazi wa tezi mbalimbali za kutengeneza homoni na kuweka sawa viwango vya homoni katika mwili. Makadiridio yasiyo rasmi yanaonyesha kuwa asilimia 25 ya watu duniani wanakabiliwa na upungufu wa zinc na kwa sababu mwili wa binadamu hauhifadhi zinc, tunalazimika kupata zinc kila siku. Vyanzo vya madini ya zinc Kwa msomaji wa makala hii, tambua kwamba huhutaji kwenda mbali zaidi kupata madini haya muhimu kwa afya yako, maana hupatikana kwenye vyalula vinavyotyuzunguka kiurahisi kama 1.Maini 2. Mboga za spinach 3. mbegu za maboga na karanga 4. nyama nyekundu 5. maharage na maziwa na