Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2017

MAUMIVU WAKATI WA TENDO LA NDOA KWA MWANAMKE.

MAELEZO YA UTANGULIZI KUHUSU TATIZO LA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA KWA WANAWAKE Nimekuwa Napata kesi nyingi sana kutoka kwa akina mama hasa  wenye umri kuanzia miaka 25 na kuendelea wakihitaji msaada kwenye ndoa zao, maana hawafurahii tendo la ndoa kama vile inavotakiwa. Tatizo linazidi kuongezeka kwa kasi na wengi hawafahamu chanzo cha tatizo hili hivo inakuwa vigumu kulitibu. Leo tutaongelea chanzo cha tatizo na jinsi ya kuepuka na kulitibu ili uendelee kufurahia unyumba. Wanawake hawakuumbiwa matatizo ya kiafya.           SABABU ZA KUPATA MAUMIVU WAKATI WA TENDO LA NDOA      KUVIMBA kwa kuta za uke kutokana na kushambuliwa na fangasi (candida Albicans) au bakteria . Kuta hizi huanza kuwa na vijitundu vidogo vidogo na kadiri muda unavyokwenda bila kutibiwa, vitundu hivi huongezeka ukubwa na kuwa kama vidonda na hatimaye kuta za uke kuanza kumomonyoka na hali hii huondoa kabisa hamu ya kushiriki tendo.    Matatizo ya shingo ya kizazi (cervical incompetence) kutokana n

JE UNATAFUTA TIBA YA MAUMIVU YA VIUNGO NA MGONGO?? SOMA MAKALA HII

Maumivu ya joint ni tatizo linalosumbua watu wengi kwa sasa kutokana na mabadiliko ya mitindo ya Maisha. Umri mkubwa ni moja ya sababu inayopelekea kutokea kwa tatizo, ambapo tishu za mwili zinakuwa kavu na kupoteza uwezo wa kuvutika. Watu wengi wanfikiri kwamba kufanya mazoezi ni hatari kwa afya ya joints lakini ukweli ni kwamba ili kuepuka magonjwa ya joints mazoezi ni lazima katika akuongeza ufanisi wa viungo pia.  Nina uhakika kuwa umewaona akina mama wenye umri mkubwa na miili mikubwa wanavyopata shida kutembea huku wakiinama toka upande mmoja hadi mwingine kila wakipiga hatua au shida wanayopata pale inapowabidi kupanda ngazi au kukuchuchumaa. Maneno kama “ugonjwa wa kuumwa joints, nina tatizo la joints, maumivu ya joints” na maumivu ya mifupa umeyasikia mara nyingi. Tatizo hasa hapa ni nini? Ungana nami katika mada hii uujue ugonjwa huu wa arthritis.   UGONJWA WA ARTHRITIS NI NINI?  Arthritis ni ugonjwa unaotokana na namna yo yote ya hitilafu katika maungio ya mifup

KUVIMBA KWA TEZI DUME (PROSTATE GLAND) NA TIBA

Kwanini Tezi Dume inavimba, Je Kuna Tiba ya Tezi Dume? Ili kujibu maswali haya na mengine mengi tuanze kwanza kwa kufahamu nini maana ya tezi dume. Tezi dume ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume. Inaundwa na sehemu mbili, lobes, ambazo zimeunganishwa na kufunikwa kwa nje kwa utando wa tishu. Tezi hii ipo mbele kidogo ya puru (rectum) na na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra).            Tezi hii ina sifa zifuatazo.                  ·       Ina umbo kama yai (oval shape)           ·   Ina ukubwa wenye vipimo hivi, upana 4cm na unene 3cm ingawaje hivi vipimo      vinatofautiana kwa kila mwanaume.           ·     Tezi hii hua yenye ukubwa wa kawaida lakini huongezeka ukubwa kadri ya umri unavoongezeka.     ·     Tezi hii hutengeneza majimaji yenye rutuba ya mbegu za kiume(shahawa) yanayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) wakati wa kilele cha tendo la ngono. Mchanganyiko huu wa mbegu pa