Skip to main content

UHUSIANO KATI YA UGUMBA NA UPUNGUFU WA MADINI YA ZINC

  Zinc ni elementi muhimu mno katika afya ya binadamu hivi kwamba ukosefu kidogo unaweza kuleta madhara makubwa. Zinc ni ya muhimu sana kwa sababu inapatikana ndani ya kila kiungo cha mwili cha binadmu na inahusika kwa karibu sana na kugawanyika kwa seli za mwili. Ni antioxidant yenye nguvu sana, inayosaidia kuzuia kansa, na pia inahusika moja kwa moja katika ufanyaji kazi wa tezi mbalimbali za kutengeneza homoni na kuweka sawa viwango vya homoni katika mwili. Makadiridio yasiyo rasmi yanaonyesha kuwa asilimia 25 ya watu duniani wanakabiliwa na upungufu wa zinc na kwa sababu mwili wa binadamu hauhifadhi zinc, tunalazimika kupata zinc kila siku.

Vyanzo vya madini ya zinc

Kwa msomaji wa makala hii, tambua kwamba huhutaji kwenda mbali zaidi kupata madini haya muhimu kwa afya yako, maana hupatikana kwenye vyalula vinavyotyuzunguka kiurahisi kama
1.Maini

2. Mboga za spinach

3. mbegu za maboga na karanga











4. nyama nyekundu
5. maharage na maziwa na
6. Uyoga na Parachichi

Baadhi ya dalili ambazo zitakusaidia kutambua kuwa una upungufu wa madini ya zinc ni pamoja na

  • Kupungua kwa uweo wa tendo la ndoa
  • Kupoteza hamu ya kula
  •  Kujiskia vibaya na huna mood mara kwa  mara
  • Kupungua kwa uwezo wa kutambua ladha ama harufu ya kitu
Kama unatambua una dalili zote hizi hapo juu basi hakikisha unaonana na dactari wako ili uweze kupata vipimo na ushauri wa kitaalamu.

Faida za madini ya zinc mwilini


  1.      Kusawazisha kiwango cha sukari katika mwili
  2.       Kusaidia utengenezwaji wa protini kwenye mwili
  3.      Kusaidia kusapoti mfumo wa upumuaji
  4.       Kuongeza ufananyaji kazi wa seli za mwili
  5.       Kupunguza sumu mwilini na kusaidia mmengeyo wa chakula

UPUNGUFU ZA ZINC NA AFYA  YA UZAZI

Upungufu wa zinc husababisha ugumba kwa jinsia zote, wanaume na wanawake na kuwasababishia tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa. Kiwango kidogo cha zinc katika mwili hukuza madhara ya msongo wa mawazo katika mwili na kuchochea uzeekaji wa haraka.
Isije ikafikiriwa kuwa upungufu wa zinc upo zaidi kwa watu wenye lishe duni au wale katika nchi zinaendelea tu. Ukweli ni kuwa tatizo hili lipo Marekani na Ulaya kwa wanaume, wanawake na watoto.
Upungufu wa zinc hubadili namna ya kusikia ladha na kusababisha kupenda chumvi zaidi, chakula kitamu zaidi. Inaweza kujidhihirisha kwa kuharisha, upungufu wa nguvu za mwili, uchovu sugu, ugumba, upungufu wa kinga za mwili, kukosa kumbukumbu, kushindwa kutuliza mawazo, kuchelewa kupona vidonda, neva kutofanya kazi vizuri, na kuunguruma kwa sauti kwenye masikio.

Afya Ya Uzazi Ya Mwanaume:

Zinc ni madini ya lazima katika kuweka testosterone kwenye kiwango kinachotakiwa, na seli za tezi dume ya mwanamme zinahitaji kiwango cha zinc ambacho ni mara 10 zaidi ya mahitaji ya seli nyingine za mwili ili ziwe na afya na zifanye kazi kwa kiwango kinachotakiwa. Upungufu wa zinc kwa wanaume huathiri uzalishaji wa testosterone, na hivo kupelekea ugumba kwa mwanaume kushindwa kumpa ujauzito mke wake,  huwaweka wanaume kwenye mazingira hatarishi ya kupata saratani ya tezi dume,. Upungufu wa zinc umehusishwa na kukosa hamu ya kufanya mapenzi.

Afya Ya Uzazi Ya Mwanamke:

Kwa wanawake, zinc inahusika katika ukuuaji wa yai (oocyte). Kama mwanamke atakuwa na upungufu wa zinc, yai halitakomaa vizuri na utolewaji wa yai (ovulation) utazuiliwa , na kusababisha ugumba. Kiwango cha zinc cha kutosha kunamwezesha mwanamke kutumia estrogen na progesterone vizuri.

Faida zingine za madini ya zinc ni pamoja na 

Kuboresha Kinga Za Mwili:

Upungufu wa Zinc unaathiri kwa kiwango kikubwa mfumo wa kinga za mwili kwa sababu upungufu huo husababisha kudorora kwa haraka kwa ufanyaji kazi wa T cell. T cells huinua kinga za mwili wakati virusi, bakteria , au changamoto nyingine zinapotokea. watu wenye umri mkubwa huwa kwenye hatari ya kuwa na upungufu, sababu kubwa ikiwa ni kukosa zinc ya kutosha kutoka kwenye milo yao. Kuna ushahidi wa kuonyesha kuwa mahitaji ya zinc huongezeka na umri ili kuzuia uvimbe, kusaidia kinga za mwili , na kuhakikisha ufanyaji kazi wa seli unaotakiwa.

Kulinda Mfumo Wa Mishipa Ya Moyo:

Zinc ni muhimu katika kuweka sawa afya ya seli za mishipa ya moyo na endothelium. Endothelium ni tabaka jembamba la seli zinazotanda juu ya mishipa ya damu na zina mchango mkubwa katika mzunguko wa damu. Kiwango kidogo cha zinc kinaweza kusababisha kuzuiwa kwa endothelium na kusababisha kuongezeka kwa cholesterol na uvimbe. Cholesterol na uvimbe huongeza uwezekano wa kutokea magonjwa ya moyo.

Kupunguza hatari ya kupata Kisukari

Zinc huhitajika katika kuhakikisha homoni nyingi zinafanya kazi vizuri, pamoja na insulin. Zinc hunata kwenye insulin na kusababisha insulin kuhifadhiwa kwa wingi ndani ya kongosho na kutolewa pale glucose inapoingia kwenye mfumo wa damu. Pili, zinc inaisaidia insulin kunata kwenye seli na kufungua mlango ili glucose iweze kuingia. Ikiwa seli hazitataka kuipokea insulin, glucose itabakia ndani ya mfumo wa damu, itasababisha kiwango cha sukari kuwa juu, na kusababisha kuongezeka kwa mafuta. Kiwango cha zinc kinaposhuka, utolewaji wa insulin utapungua na pia upokewaji wa insulin hiyo, ambapo hali ikiendelea, tatizo la kisukari hutokea. Utafiti wa hivi karibuni huko Hispania uliohusisha wanafunzi ulionyesha uhusiano wa moja kwa moja kati ya upungufu wa zinc, uwingi wa mafuta mwilini, na mwili kutoipokea insulin.

Kiondoa Sumu Chenye Nguvu

Kudorora kwa afya ya neva na ugonjwa wa Alzheimer's huchochewa na kujikusanya kwa metal nzito katika ubongo. Zinc husaidia kuondoa sumu hizi na kusaidia katika kuboresha ufanyaji kazi wa seli za ubongo (cellular homeostasis). Zinc ina mchango mkubwa sana katika shughuli za mawasiliano baina ya neva na husaidia kuweka sawa afya na umbo la ubongo. Pia, zinc ni sehemu ya kimeng'enya kinachohusika katika kuvunjavunja mafuta katika ngozi nyembamba inayofunika ubongo. Hii ni kazi muhimu sana kwa sababu katika kutunza afya ya ubongo na ufanyaji wake kazi, inatakiwa kuhakikisha kuwa ngozi hii nyembamba inapata virutubisho inavyovihitaji.

Kuzuia kutoka kwa saratani

Kuweka viwango vizuri vya zinc katika miili yetu kumeonyesha kuwa kunaweza kusaidia kuponya matatizo mengi sugu ya kiafya, hasa kansa na upungufu wa kinga za mwili. Pamoja na kansa ya tezi dume, upungufu wa zinc umeonyesha kuhusika sana katika kujenga karibu aina zote za kansa. Utafiti wa hivi karibuni umehusisha upungufu wa zinc na kansa za maziwa, utumbo mkubwa, ovari, mapafu , ngozi, na leukemia.                       
NB, kama una matatizo ya ugumba na kutopata motto basi nashauri mke na mume wafike kituo cha afya wote wawili waweze kupata vipimo ili kujua chanbzo cha tatizo hapo ndipo wanaweza kuanza kutumia dawa.


 Kwa wale akina mama wenye matatizo ya homoni, kuvurugika kwa hedhi na kukosa ujauzito kwa mda mrefu basi tumewaandalia programme ya week 3 ambayo itakusaidia kubalansi homoni zako na kurejesha uwezo wa kushika ujauzito. Tunashauri wanandoa wote kufanya vipimo ili kujua chanzo cha tatizo lako la kushindwa kushika ujauzito. karibu nawe upate huduma hii ya virutubisho na dawa zetu za asili ili uwe mmoja wa mashuhuda na mwenye furaha kama baadhi ya hawa wagonjwa tuliokwisha kuwapa huduma.

UTAFITI UNASEMAJE KUHUSU TIBA NA VIRUTUBISHO VYA KUSAWAZISHA HOMONI ZA KIKE.

1. Zinc capsules

Kwa wanawake, MADINI YA ZINC yanahusika katika ukuuaji wa yai (oocyte). Kama mwanamke atakuwa na upungufu wa zinc, yai halitakomaa vizuri na utolewaji wa yai (ovulation) utazuiliwa , na kusababisha ugumba. Kiwango cha zinc cha kutosha kunamwezesha mwanamke kutumia estrogen na progesterone vizuri. hakikisha unapata virutubisho kutoka kwenye vyanzo vilivyothibitishwa.

2. Soy capsules

vidonge hivi vilivyotengenezwa kiasili kwa kutumia viambata vya mimea ya Semen Glycine, Radiz Paeoniae Alba Eztractum na Ganoderma husaidia: kuongeza ufanyaji kazi wa mfuko wa mayai (ovaries), kuzuia Saratani ya matiti, kuimarisha afya ya mifupa kwa wanawake waliokoma hedhi.(menopause). 

Shuhuda za Wagonjwa Kushika Ujauzito baada ya Kutumia Zinc, Vig power na Soy power



     Naamini nawe unatamani kufikia malengo haya na umehangaika hospitali nyingi bila msaada, basi anza kurejesha tumaini lako. 
      Unaweza kuwa wewe ni mzima hivo mfahamishe na mwingine kuhusu huduma hii. karibu.

Maelezo ya mwisho

Kwa wagonjwa wenye shida katika kushika ujauzito, tunawashauri kufanya vipimo wote wawili mke na mume ili kujua chanzo cha tatizo. Baada ya hapo tunaweza kuwaanzishia huduma yetu

VIRUTUBISHO VYOTE HIVI VINAPATIKANA OFSINI KWETU MAGOMENI MWEMBECHAI  KWA

 GHARAMA YA JUMLA SH 150,000/= . Hivo huhitaji kuagiza nje ya nchi, tayari tumefanyia vipimo na vimethibitishwa kutibu matatizo ya ugumba na homoni.


Bofya hapa Kuchati na Daktari kwa Whatsapp uagize dawa 





Comments

Popular posts from this blog

KUTOKWA NA UCHAFU UKENI, CHANZO NA TIBA YAKE

Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke. Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi. Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke. Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili. Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha. Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eno la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni. Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa. Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke. Uchafu Wa Sehemu Za Siri  Wa Kawaida Wanawake wote hutoa uchafu sehemu za siri. Kiwango cha uchafu unaotoka, ra

JINSI YA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATIZO YATOKANAYO NA KUKUA KWA TEZI DUME KWA KUTUMIA VYAKULA HIVI VI 5

Maelezo ya utangulizi. Kichocheo cha testosterone, japo huusishwa zaidi na upande wa mwananume ni muhimu kwa afya ya pande zote mbili yaani mwanamke na mwanamme pia.kadiri umri unavoenda mbele basi kiwango cha uzalishaji wa kichocheo cha testerone kupungua, kupungua kwa kichocheo hiki kunaambatana na ukuaji wa tezi dume (prostate gland),kupotea kwa nywele na pia saratani mfano saratani ya tezi dume. .KAZI KUBWA YA KICHOCHEO HIKI NI KUONGEZA MSUKUMO NA HAMU YA TENDO LA NDOA , KUIMARISHA MISULI NA MIFUPA MWILINI. NINI KINAHITAJIKA ILI KUZALISHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE? Ili kuhakikisha uzalishaji wa kichocheo cha kiume unafanyika, mwili unahitaji virutubisho au viini lishe mbalimbali, baadhi ya viini lishe hivyo ni madini ya ZINC na vitamin D3,  vitamini D inaweza kuzalishwa na mwili pale ngozi yako inapokutana na mwanga wa jua, hapa nazungumzia mwanga wa asubuhi wakati jua ndo linachomoza na pia lile jua la jion karibia na kuzama, hivyo utakubaliana na mimi kuwa wengi wet

MADHARA YA PUNYETO NA TIBA YAKE

MAELEZO  YA AWALI KUHUSU TATIZO LA UPIGAJI PUNYETO Watu wengi sana wanataka kufahamu jinsi gani wafanye ili kuachana na kitendo cha upigaji punyeto. Punyeto ni tendo la mtu la kuamsha hisia za mapenzi au msisimko ambao unampelekea mtu huyu kufikia kilele cha kujimalizia tamaa zake! Bila kufanya tendo halisi, hutumia fikra zake katika picha za zinazoitwa za ngono au picha zozote zinazoweza kulifanikisha tendo hilo, movie n.k. Kilele cha yote anafikia mahali anajimalzia tamaa zake mwenyewe!. Nimekuwa nikiona baadhi ya watu wanaosema wameelimika wakipingana wao kwa wao katika suala zima la kupiga punyeto! Wako wanaotetea kutokana na elimu yao na wanasema kwa ujasiri mkubwa kwamba "kupiga punyeto ni sehemu ya maisha ya mwanadamu" Ina maana katika maisha ya mwanadamu upigaji punyeto inaelezwa ni kama tendo la lazima mpaka inafikia mahali wanasema ni sehemu ya maisha (Maisha) ya mwanadamu. Nimekuwa nikipata kesi nyingi sana juu ya madhara yatokanayo na punyeto. Aslimia 60