Skip to main content

SAYANSI YA CHAKULA CHA WANGA NA SUKARI NA MSTAKABALI WA AFYA YAKO

Moja ya vyakula ambavyo tumekuwa tukitumia kwa wingi sana hasa kwa watanzania wenye kipato cha kati na chini kabisa ni vyakula vya aina kuu tatu, WANGA,PROTINI NA MAFUTA (FATS). Na kwa kiwango kidogo sana tunatumia vitamin na madini katika miili yetu. Na moja ya masomo ya chakula tunayofundishwa ni kula MLO KAMILI. Na ndio watu wengi tumekuwa tukitumia elimu hio hadi hapa tulipo fika. Lakini basi napenda kusema tu kwamba mlo kamili ni kwa ajili ya mtu mzima ambaye hana ugonjwa wowote na ni kwa yule tu ambaye hataki kula kiafya.
 Napenda kusema haya kwa sababu tumekuwa tukila vyakula vya namna ile ile lakini tumekuwa tukiugua sana magonjwa mbalimbali yatokanayo na lishe mbovu. Na hadi sasa ugonjwa wa kisukari hapa duniani unaua sana Zaidi ya ugonjwa wa HIV sasa ni swala la kujiuliza tunakosea  wapi mbali katika lishe?
Leo nataka nikueleze kidogo kuhusu sayansi ya chakula aina ya wanga. Maana kila mtu ninayemwelekeza njia sahihi ya kupunguza uzito anakwambia nitaishije bila chakula cha wanga? Mwili wako hutumia vyakula vikuu aina tatu ambavyo ni wanga,protini na fats. Na unatakiwa ujue kuwa gramu moja ya wanga hutengeneza nishati ya mwili kalori 4, ambapo protini nayo hutengeneza kalori 4 na Fats hutenegenza kalori 9. Unaona ni Zaidi ya mara mbili ya nishati zinazotengenezwa na chakula cha wanga. Hii ina maana kuwa ninaposema kuwa tunaweza kupunguza wanga na ukaishi ukiwa na nguvu nyingi Zaidi hata ya ulivyo kuwa katika lishe ya wanga nyingi.

KWA NINI NAKUSHAURI UPUNGUZE WANGA NA SUKARI KIAFYA?
Unapokuwa umepunguza wanga na sukari au kuacha kabisa ulaji wa vyakula vyenye wanga nyingi, mfano mikate,ugali,wali,tambi nk na hakikisha kitendo hicho kiendane na kuongeza kiwango cha mafuta na vyakula vya protini mwilini mwako katika lishe yako. Hii itaufanya mwili wako kuanza kutumia mafuta kama nishati ya mwili ya kwanza kujitengenezea nishati. Na viungo vya binadamu kama Ini na figo vinapokuwa vinatumia mafuta kuzalisha nishati ya mwili hutenegeneza viini vya nishati viitwavyo KETONE BODIES, ambavyo hivi ndivyo hutumiwa na seli za mwili kujitengenezea nishati kwa wingi.
Hivyo basi unapokuwa unajizuia kutumia vyakula vya wanga mwili wako utatumia karibia siku 5 hadi wiki kuanza kutumia mafuta kama nisharti ya mwili na hicho kitendo tunaita KETO ADAPTATION. Ningependa kusema kwamba KETO ADAPTATION ni ile hali mwili wako kujenga mazoea ya kutumia mafuta kama chanzo cha nishati ya mwili na hapo ndipo utaanza kuona mabadiriko katika mwili wako makubwa sana.
Utakuwa unajisikia mwenye nguvu na unatashangaaa dalili mbalimbali zilizokuwa zinakusumbua zinapotea hii ni kwa sababu ya uwezo mkubwa wa ketone bodies katika mwili wako dhidi ya glucose.
Sote tunajua kwamba ulaji wa vyakula vya wanga kwa wingi na vyakula vyenye sukari nyingi vinaongeza kiwango cha sukari kwenye damu Zaidi ya kiwango ambacho mwili wako unaweza kuhimili.
Mfano, Kiwango cha kawaida cha sukari kinachohitajika mwilini mwako ni kijiko kimoja cha chai, hiki ni kiwango ambacho hakiwezi kukuletea matatizo. Basi kama binadamu anaishi kwa sukari inayokadiriwa kuwepo kwenye damu kama kijiko kimoja tu cha chai. Unywaji wa soda moja unaweza kuongeza Zaidi ya vijiko 10 hivyo basi mwili wako unakuwa unashindwa kuhimili sukari iliyozidi. Na ulaji wa Baga inakadiliwa kuwa baga moja ya kati inaweza kutoa sukari Zaidi ya vijiko 16 kwenye damu. Swali la kujiuliza mwili unapeleka wapi sukari iliyozidi wakati miili yetu inahitaji sukari kiwango kidogo sana kama kijiko kimoja tu kuishi?
Mwili hutengeneza maji kutoka kwenye seli za  kongosho ziitwazo beta seli,maji haya ni homon iitwayo INSULIN
Kazi kubwa ya insulin ni kutunza glucose hii katika damu kwa matumizi ya baadae, na inatunza katika kiasi maalumu katika mfumo wa Glycogen na kiasi kikubwa katika mafuta. Na hivyo basi mafuta haya huhifadhiwa katika sehemu mbalimbali kama tumboni,shingoni,mikononi,kifuani,kiunoni nk. Na mafuta haya huhifadhiwa katika mfumo wa TRYGLYCERIDES ambayo haya ni miongoni vya mafuta mabaya mwilini mwako. Sasa mtu anayekwambia wanga nyingi katika chakula chako ni salama anakudanganya kwa kiasi kikubwa kwani tunaona jinsi gani ulaji wa kiwango kingi cha vyakula vya wanga na sukari vinavyo sababisha sukari kupanda kupita kiasi na insulinkuanza kuhifadhi katika mafuta.
Kila siku nasema, tumekaririshwa adui mkuu ni fats, na kujisahau ulaji mbovu wa vyakula vya wanga na hatimaye tumeishia kulea vitambi na magonjwa sugu hii yote ni kutokuwa na ufuatiliaji wa lishe nzuri na salama kwako.

NINI MADHARA MENGINE YA SUKARI KUWA KATIKA KIWANGO KIKUBWA KUZIDI MAHITAJI YA KAWAIDA YA MWILI?
Napenda kuwarudisha nyuma kidogo katika somo la bailojia. Tulijifunza kuwa miili yetu umejengwa kwa kiini kidogo sana kiitwacho SELI ambapo shughuli zote za mwili zinafanyika humo. Na nilipo fika mbali Zaidi katika bailojia nilijifunza kuwa ndani ya seli kuna viungo vidogo vidogo navifananisha na ( Apartments  kwenye nyumba kubwa) moja wapo ni MITOCHONDRIA, hiki ni kiungo kidogo sana katika seli ambacho kinahusika na kuzalisha nishati ya mwili tu.
Mfano, una nyumba yako kubwa sana na hio nyumba ukaitenga kuwa ya biashara na kila chumba ukakiwekea majukumu yake na mitambo yake. Hivyo basi kile chumba kimoja ukakiwekea mitambo ya kufua umeme na ndicho kitafanya shughuli zote zifanyike katika kiwanda chako ndani ya hio nyumba ya kibiashara. Hicho chumba cha kufua umeme nakifananisha na MITOCHONDRIA ndani ya seli ya binadamu ambayo hushughurika na kutenegeneza nishati ya mwili ndani ya seli.

Pia nikikumbuka watu wote tulijifunza kwamba mwili wetu hujitenegenezea nishati ya mwili au nguvu kupitia kuifanyia kazi sukari iliyo ndani ya damu baada ya kuingia ndani ya seli. Hivyo basi insulin ni kama ufunguo ambao unafungua milango ili sukari iweze kuingia ndani ya seli hadi kwenye mitochondria. Baada ya kufika huko, mwili huanza kuzalisha nishati na kuitoa katika mfumo wa ATP kupitia kitendo cha AEROBIC RESPIRATION. Kitendo hiki hufanyika ndani ya seli ndani ya mitondria kwa kuwepo na hewa ya oxygen. Hewa hii lazima iwepo ili mwili uweze kuzalisha nishati ya kutosha uweze kufanya kazi mbalimbali.

Mwili wako unapokuwa unatumia hewa ya oxygen kuna uwezekano mkubwa wa kupatikana kwa athari iitwayo OXDATIVE STRESS. Hii ndio inayofanya chuma ipate kutu, hii ndio inayofanya mafuta ukiyaweka kwenye jua kwa muda mrefu yanaharibika. Basi mwili wako unakuwa unatengeneza vihatarishi viitwavyo REACTIVE OXYGEN SPECIES kwa kifupi huitwa FREE RADICALS. Hizi free radicals ni sumu ambazo hupatikana wakati mwili unajitenegenezea nishati yake kwa kutumia oxygen na hizi zinapokuwa kiwango kikubwa huweza kuharibu kabisa seli na kuziua na pia zinaweza kupelekea kupata magonjwa sugu kama kansa nk. Hivyo tafiti zinaonesha kwamba vyakula vya wanga na sukari vina matokeo makubwa ya kutenegeneza FREE RADICALS nyingi kupita kiasi. Miili yetu ina kiwango flani cha viondoa sumu ambavyo vinaipunguza  sumu ya free radicals kuepusha kusababisha magonjwa kwa kuziua seli. Lakini panapokuwa na kiwango kikubwa cha uzalishaji wa free radicals mwili unashindwa kuhimili na hatimaye free radicals zinaanza kuleta madhara mwilini mwako. Kadri mitochondria zinavyo dhoofika ndivyo magonjwa nyemelezi ya lishe yanavyotukabili kila kukicha.

MADHARA YA FREE RADICALS
1. Hudhoofisha seli zako na kusababisha mwili kutofanya kazi ipasavyo
2. Huua kabisa seli za mwili
3. Huweza kubadili seli za mwili wako na kuwa kansa

Pili kunapokuwa na sukari nyingi katika damu, sukari nyingi katika damu huwa ipo katika mfumo wa kimiminika mfano wa dawa za maji  za watoto (syrup) au juisi ya embe inayokumwagikia mkononi chukulia mfano huo. Sukari iliyozidi huungana na protin katika tishu za mwili na kutenegeneza kitu kiitwacho GLYCATION. Muungano huo ufanya protini zisiweze kufanya kazi na hatimaye kuishia hatua ya mwisho iitwayo ADVANCED GLYCATED END PRODUCTS (AGEs) ambacho ni kiini kinacho ambatana na magonjwa mengi, magonjwa ya kusau,magonjwa ya kisukari,magonjwa ya kutetemeka uzeeni,baridi yabisi,upungufu wa nguvu za kiume,maumivu ya misuli,uchovu wa muda mrefu,macho kutoona vizuri nk. Advanced Glycated end products pia ndio chanzo kikubwa kinacho ua nguvu za macho kwa wagonjwa wa kisukari,figo,miguu kufa ngazi nk

FAIDA YA MWILI KUTUMIA FATS KUZALISHA NISHATI YA MWILI
1. Mwili unakuwa una nguvu za kutosha unapokuwa unatumia fats au ketone bodies kuzalisha nguvu
2. Mwili unapokuwa unatumia mafuta kuzalisha nishati hupunguza kiwango cha cha FREE RADICALS MWILINI
3. Vyakula vya Protini,mafuta vinaonesha kutopandisha kiwango cha insulin (Kihifadhi mafuta) kwa kiwango kikubwa kama ilivyo vyakula vya wanga
4. Utajitibu magonjwa mengi sana kwani utazuia utenegenzwaji wa FREE RADICALS na Advanced Glycated End Products ambavyo ni vyanzo vya magonjwa mengi ambapo chanzo chake ni ulaji wa vyakula vya wanga kwa wingi kupita kiasi.

FIKRA POTOFU ZITAKAZO KUPOTOSHA KATIKA SAFARI YAKO KIAFYA
Najua kuna watu wanashangaa kwa nini nasema kuwa ili uweze kushusha uzito na kitambi lazima tupigane vita na wingi wa vyakula vya wanga katika mlo wako na sio mafuta kama wengi tulivyokaririshwa. Adui yetu mkuu ni sukari na huyo kila siku tumpinge na rafiki yetu katika kupunguza uzito ni vyakula vya mafuta,protini,mboga za majani na baadhi ya matunda hasa yenye nyuzi nyingi.

1. Wataalamu wengine watakuambia Ubongo hautumii chanzo cha nishati yoyote isipokuwa wanga? Sasa wewe unaye acha wanga utaishi vipi? Hii ni kauli inatufanya tuzidi kulea vitambi kila siku.
Ni kweli ubongo,seli za retina za jicho na seli za figo hutegemea sukari itokanayo na wanga kuzalisha nishati ya kufanyia kazi. Lakini napenda kusema kuwa usigubikwe na uelewa mdogo wa sayansi ya kupungua uzito wa mtaalamu wako. Napenda kukuambia kuwa, ili mwili wako ubadirilke uwe machine inayo unguza mafuta tunashauri kiwango cha wanga kiwe chini ya gramu 50 tu. Yani namaanisha kuwa hicho kiwango utakipata katika vyakula vyenye kiwango kidgo cha wanga kama mboga za majani,protini na baadhi ya matunda nitakayo kuruhusu utumie na sio upotoshaji kwamba ule kaugali kadogo kumaanisha kuwa unatumia wanga kidogo! Wanga utaipata kwenye aina zingine za vyakula. 
Hivyo basi ubongo wako utaishi hai kwa kutumia wanga ambao utaipata kwenye mboga za majani,protini na baadh ya matunda ambapo si Zaidi za gramu 50 utapata. Kiasi kingine mwili huzalisha glucose kwa njia kuu mbili kwenye Ini la binadamu, Gluconeogenesis na Glycogenolysis hivyo mwili wako utapata nishati za kutosha kwa zile seli zinazotegemea glucose kufanya kazi. Na hio ndiyo sayansi ya kupungua uzito, kwamba mwili ukisha maliza kutumia chakula cha protini ,mafuta ulicho kula, basi mwili utaanza kutumia mafuta yaliyohifadhiwa kama nyama uzembe na hapo ndipo mwili wako utabadirika kuwa mashine inayo unguza mafuta. Na sio kuhifadhi mafuta tena maana hakuna sukari inayozidi kwenye damu, sukari yote inayopatikana inatumka kuendesha shughuri za mwili.

2. Wataalamu watakwambia Ketone bodies ambazo ni vyanzo vya nishati ambavyo huzalishwa pale mwili unapotumia mafuta kama chanzo cha nishati ni sumu kwenye neva za fahamu na hatari sana.
Hii nimekuwa nikisikia wataalamu baadhi wanajaribu kuoanisha jinsi gani elimu ya ketones bodies kwa watu wenye kisukari aina ya kwanza inavyo wapata. Ukweli ni kwamba ketone bodies ndio chanzo cha pekee kinachokufanya hata leo hii upo hai. Kama ingekuwa sumu ungekuwa basi hatupo na wewe hapa duniani kwa sababu unapokuwa hujala angalau masaa 8 mpaka 16 mwili wako huanza kuzalisha niashati mbadala kutokana na ketones kwa sababu sukari imeisha mwilini.
Sasa kumbuka mwili wako unatumia ketone huku kiwango chako cha insulin kipo sawa na kiwango kinacho jitosheleza, na kwa wagonjwa wakisukari aina ya kwanza huzidiwa na ketone bodies kwa sababu huwa hawana kabisa insulin kwenye damu yao.
Sasa je unaona utofauti hapo, ketone zinazotumika wakati una insulin ya kutosha na ketone inapozalishwa kwa mtu ambaye hana insulin ya kutosha.Hivyo basi nazani umeelewa jinsi gani tunavyoishi kwa kutumia kiini hiki cha nishati baada ya mwili kukaa muda mrefu hujala badi unatafuta njia mbadala wa kutumia mafuta kuzalisha nishati ya mwili. Sasa iweje leo hii ketone ni sumu? Usipotoke soma upate maarifa ya sayansi ya kupungua uzito.

3. JE AINA HII YA MLO NI SAWA NA KUJINYIMA KULA (STARVATION)?
Kujinyima kula kunafanya uzito kuongenezeka kwa kasi ya ajabu, hii ni kwa sababu unapokuwa umekaa muda mrefu bila kupata chakula mwili wako unatenegeneza homoni ziitwazo stress homones ambazo ni pamoja na Cortisol hii inakufanya ulaji hovyo na kuongezeka uzito tofauti na ulivyotarajia.
Na mlo huu una utofauti sana na kujinyima maana kujinyima ni kutokula chakula chochote ambazo sivyo ninavyofundisha mimi kila siku.
Unapokuwa huli,umefunga labda siku 5 mwili wako utaanza kutumia protini za kwenye misuli na hatimaye mwili kuanza kudhoofika, hio ni hali ya kutopungua kiafya. Lakini kama ukifuatilia mlo huu, mwili utaanza kwanza kutumia lishe ambayo umekula kama mboga za majani,protini, na fats kwa wingi na baada ya hapo mwili utaanza kuunguza mafuta. Namaanisha kuwa mwili wako utatumia lishe uliyokula na baada ya hapo utaanza kuunguza mafuta, Je ni sawa na mtu yaliyefunga? Hapana! Ninachokushauri jifunze sayansi ya kupungua uzito na lishe kwa ujumla.

MAMBO YA KUZINGATIA
1. Najua umekuwa ukijitahidi kujinusuru na uzito mkubwa na magonjwa mengi, lakini umekuwa mvivu wa kuamini lishe yako ndio chanzo cha magonjwa yako yote uliyo nayo, ndio maana umekuwa ukitibu dalili za magonjwa yako sugu badala ya kushughurikia tatizo kuanzia kwenye seli na jinsi gani lishe zinavyofanyiwa kazi ndani ya seli.
2. Wengi wetu ni wavivu wa kutunza afya zao na wanaona kuwa wanastahili kuwa katika hali hizo ambapo sio kweli, maana uzito huo hukuzaliwa nao,kitambi hicho hukuzaliwa nacho, kwa nini leo iwe kama ni medali ya ukubwani? Naona uchukue hatua kunusuru afya yako.

UKITAKA KUTIBU MAGONJWA MENGI TABIA, AU MAGONJWA YA LISHE MBOVU ANGALIA CHANZO CHAKE KUANZIA KWENYE SELI JINSI GANI VIINI LISHE VINAVYOFANYIWA KAZI.

SHARE NA MARAFIKI ZAKO MAKALA HII ILI WAPATE KUELIMIKA ZAIDI.
na ukiwa na swali ama maoni usisite kutuandikia kwa namba yetu 0762336530.

Comments

Popular posts from this blog

KUTOKWA NA UCHAFU UKENI, CHANZO NA TIBA YAKE

Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke. Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi. Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke. Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili. Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha. Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eno la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni. Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa. Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke. Uchafu Wa Sehemu Za Siri  Wa Kawaida Wanawake wote hutoa uchafu sehemu za siri. Kiwango cha uchafu unaotoka, ra

JINSI YA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATIZO YATOKANAYO NA KUKUA KWA TEZI DUME KWA KUTUMIA VYAKULA HIVI VI 5

Maelezo ya utangulizi. Kichocheo cha testosterone, japo huusishwa zaidi na upande wa mwananume ni muhimu kwa afya ya pande zote mbili yaani mwanamke na mwanamme pia.kadiri umri unavoenda mbele basi kiwango cha uzalishaji wa kichocheo cha testerone kupungua, kupungua kwa kichocheo hiki kunaambatana na ukuaji wa tezi dume (prostate gland),kupotea kwa nywele na pia saratani mfano saratani ya tezi dume. .KAZI KUBWA YA KICHOCHEO HIKI NI KUONGEZA MSUKUMO NA HAMU YA TENDO LA NDOA , KUIMARISHA MISULI NA MIFUPA MWILINI. NINI KINAHITAJIKA ILI KUZALISHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE? Ili kuhakikisha uzalishaji wa kichocheo cha kiume unafanyika, mwili unahitaji virutubisho au viini lishe mbalimbali, baadhi ya viini lishe hivyo ni madini ya ZINC na vitamin D3,  vitamini D inaweza kuzalishwa na mwili pale ngozi yako inapokutana na mwanga wa jua, hapa nazungumzia mwanga wa asubuhi wakati jua ndo linachomoza na pia lile jua la jion karibia na kuzama, hivyo utakubaliana na mimi kuwa wengi wet

MADHARA YA PUNYETO NA TIBA YAKE

MAELEZO  YA AWALI KUHUSU TATIZO LA UPIGAJI PUNYETO Watu wengi sana wanataka kufahamu jinsi gani wafanye ili kuachana na kitendo cha upigaji punyeto. Punyeto ni tendo la mtu la kuamsha hisia za mapenzi au msisimko ambao unampelekea mtu huyu kufikia kilele cha kujimalizia tamaa zake! Bila kufanya tendo halisi, hutumia fikra zake katika picha za zinazoitwa za ngono au picha zozote zinazoweza kulifanikisha tendo hilo, movie n.k. Kilele cha yote anafikia mahali anajimalzia tamaa zake mwenyewe!. Nimekuwa nikiona baadhi ya watu wanaosema wameelimika wakipingana wao kwa wao katika suala zima la kupiga punyeto! Wako wanaotetea kutokana na elimu yao na wanasema kwa ujasiri mkubwa kwamba "kupiga punyeto ni sehemu ya maisha ya mwanadamu" Ina maana katika maisha ya mwanadamu upigaji punyeto inaelezwa ni kama tendo la lazima mpaka inafikia mahali wanasema ni sehemu ya maisha (Maisha) ya mwanadamu. Nimekuwa nikipata kesi nyingi sana juu ya madhara yatokanayo na punyeto. Aslimia 60