Skip to main content

MATUMIZI SAHIHI YA MAJI KWA AFYA YA MWILI WAKO.


“KUNYWA MAJI MENGI” ni msisitizo ambao umekuwa ukipewa mara nyingi labda na mama nyumbani, ama na Daktari wako au rafiki wako wa karibu, lakini ambacho hukuambiwa ni kwanini maji ni muhimu kwa afya yako na pia kiasi cha maji unachotakiwa kunywa na ubora wa maji vyote ni muhimu kufahamu. Najua swali la watu wengi ni kwamba Je ni kiasi gani cha maji unachotakiwa kunywa kila siku?? . Maji ni muhimu sana kwa afy zetu ni dhahiri kwamba unaweza kuishi bila chakula kwa siku nyingi lakini bila maji utaishi mud mfupi sana. Miili yetu kiujumla imetengenezwa kwa maji ambayo
1.      Ni muhimu katika kurahisisha umeng’enyaji wa chakula, uvyonzwaji wa virutubisho na pia utoaji wa takamwili.
2.      Kusaidia usafirishaji wa vitu mbalimbali kwenye mwili.
3.      Kurekebisha joto la mwili
4.      Kulainisha joint ili kupunguza msuguano wa mifupa na
5.      Kusafisha ngozi ya mwili
KIASI GANI CHA MAJI NATAKIWA KUNYWA??
Japo kila siku unapoteza maji kwa njia ya mkojo na jasho, maji yanayopotea yanatakiwa kufidiwa. Cha kufurahisha ni kwamba mwili umeumbwa na njia inayokwambia ni muda gani ufidie hayo maji yaliyopotea, njia hii huitwa “KIU”. Inawezekana ushauri mwingi ulopata ukikwambia kunywa lita 2 ama 3 ama 4 za maji kila siku japo ni vizuri lakini siyo ushauri sahihi. UKWELI ni kwamba hakuna kiwango kimoja ambacho kinaweza kutumika na watu wote, chukulia mfano Mcheza mpira ambaye kila siku asubuhi na jioni anapiga mazoezi kipindi cha kiangazi,na mzee wa miaka 50 ambaye hafanyi mazoezi, na mama mwenye kilo 100 wakati wa kipindi cha baridi, ni dhahiri kwamba watu hawa watatu watakuwa na ujazo tofauti kabisa katika kunywa  maji.
Hivo nashauri kwamba usikilize mwili wako unasemaje katika kuamua kiwango cha maji yanayotakiwa, pale unapopata kiu basi kunywa maji kukata kiu na usinywe soda. Njia nyingine ya kugundua uhitaji wa maji kwenye mwili ni kuangalia rangi ya mkojo, mkojo ukiwa na rangi ya Njano ilokolea basi inaonyesha kwamba una uhitaji mkubwa wa kunywa maji, ;lakini kama ni njano nyepesi basi upo sawa. NB kama unameza vidonge vya vitamin B2 basi hutaweza kufanya jaribio hili maana vidonge hivi huweza kubadilisha mkojo na kuwa njano nyepesi isiyokolea. Inashauriwa pia kunywa maji kidogo kidogo na siyo kubugia glas nyingi kwa mara moja, kutokana na ukubwa wa mwili miili yetu ina uwezo wa kutumia maji kidogo kidogo, hivo ukinywa maji mengi kwa mara moja yatatumika kidogo na mengine yatatolewa nje kama uchafu.
FANYA KIU KUWA NI MWONGOZO WAKO WA KUNYWA MAJI
Mwili unapokuwa umepoteza maji asilimia 2 mpaka 3 basi hutoa alam ambayo ni kwa njia ya kiu kukwambia kwamba unatakiwa kunywa maji. Kam una afya njema basi hakikisha unakunywa maji kila unapopata kiu na hiyo ndo itakuwa mwongozo wako wa kiasi gani cha maji uweze kunywa. Ni dhahiri kwamba kama unaishi kwenye maeneo ya joto mfano maeneo ya pwani au unafanya sana mazoezi au shughuli nzito utahitaji kunywa maji mara nyingi zaidi.

MAJI NA SIYO SODA  NDO IWE KIKATA KIU YAKO, Maji safi na salama ni kinywaji kizuri kukata kiu yako na kuujenga mwili, kama umeshakuwa mnywaji wa kupindukia wa soda basi ni vizuri ukafanya mabadiliko.

Comments

Popular posts from this blog

KUTOKWA NA UCHAFU UKENI, CHANZO NA TIBA YAKE

Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke. Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi. Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke. Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili. Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha. Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eno la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni. Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa. Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke. Uchafu Wa Sehemu Za Siri  Wa Kawaida Wanawake wote hutoa uchafu sehemu za siri. Kiwango cha uchafu unaotoka, ra

JINSI YA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATIZO YATOKANAYO NA KUKUA KWA TEZI DUME KWA KUTUMIA VYAKULA HIVI VI 5

Maelezo ya utangulizi. Kichocheo cha testosterone, japo huusishwa zaidi na upande wa mwananume ni muhimu kwa afya ya pande zote mbili yaani mwanamke na mwanamme pia.kadiri umri unavoenda mbele basi kiwango cha uzalishaji wa kichocheo cha testerone kupungua, kupungua kwa kichocheo hiki kunaambatana na ukuaji wa tezi dume (prostate gland),kupotea kwa nywele na pia saratani mfano saratani ya tezi dume. .KAZI KUBWA YA KICHOCHEO HIKI NI KUONGEZA MSUKUMO NA HAMU YA TENDO LA NDOA , KUIMARISHA MISULI NA MIFUPA MWILINI. NINI KINAHITAJIKA ILI KUZALISHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE? Ili kuhakikisha uzalishaji wa kichocheo cha kiume unafanyika, mwili unahitaji virutubisho au viini lishe mbalimbali, baadhi ya viini lishe hivyo ni madini ya ZINC na vitamin D3,  vitamini D inaweza kuzalishwa na mwili pale ngozi yako inapokutana na mwanga wa jua, hapa nazungumzia mwanga wa asubuhi wakati jua ndo linachomoza na pia lile jua la jion karibia na kuzama, hivyo utakubaliana na mimi kuwa wengi wet

MADHARA YA PUNYETO NA TIBA YAKE

MAELEZO  YA AWALI KUHUSU TATIZO LA UPIGAJI PUNYETO Watu wengi sana wanataka kufahamu jinsi gani wafanye ili kuachana na kitendo cha upigaji punyeto. Punyeto ni tendo la mtu la kuamsha hisia za mapenzi au msisimko ambao unampelekea mtu huyu kufikia kilele cha kujimalizia tamaa zake! Bila kufanya tendo halisi, hutumia fikra zake katika picha za zinazoitwa za ngono au picha zozote zinazoweza kulifanikisha tendo hilo, movie n.k. Kilele cha yote anafikia mahali anajimalzia tamaa zake mwenyewe!. Nimekuwa nikiona baadhi ya watu wanaosema wameelimika wakipingana wao kwa wao katika suala zima la kupiga punyeto! Wako wanaotetea kutokana na elimu yao na wanasema kwa ujasiri mkubwa kwamba "kupiga punyeto ni sehemu ya maisha ya mwanadamu" Ina maana katika maisha ya mwanadamu upigaji punyeto inaelezwa ni kama tendo la lazima mpaka inafikia mahali wanasema ni sehemu ya maisha (Maisha) ya mwanadamu. Nimekuwa nikipata kesi nyingi sana juu ya madhara yatokanayo na punyeto. Aslimia 60