Skip to main content

MIKAKATI 7 YA KIAFYA UNAYOTAKIWA KUTEKELEZA 2017

Heri ya mwaka mpya 2017. Je umeshaweka mipango yako ya mwaka huu?? Watu wengi wameshafanya hivo lakini pia asilimia kubwa wanawahi kukata tamaa na kupunguza juhudi kuelekea kutimiza malengo yao  ifikapo mwezi wa 2 ama wa 3. Nashauri mwaka huu jikite katika kulinda fya yako kwa kubadili mtindo mbovu wa maisha na baadhi ya tabia hatarishi. Kubadili mtindo wa maisha ni suala endelevu na siyo kitu cha kutimiza siku moja au week chache .
MIKAKATI 7 YA KIAFYA UNAYOTAKIWA KUTEKELEZA 2017

1.       ACHA KUNYWA SODA NA VINJWAJI VILIVOSINDIKWA
Hii ni kwa sababu soda ina uhusiano na matatizo kama uzito mkubwa, magonjwa ya moyo, magonjwa ini,  na pia matatizo yamifupa, kama bado unatumia soda mara kwa mara basi badilisha kwa kutumia maji, kahawa na juisi ambayo umetengeneza mwenyewe nyumbani.
2.       KULA PARACHICHI KILA SIKU
Parachichi ni tunda linalopatikana kirahisi na ni chanzo cha  mafuta mazuri ambayo mwili huweza kuunguza kiurahisi ili kutoa nishati, tafiti zinasema kwamba unapoweka parachichi kwenye saladi yako basi unaongeza uvyonzaji wa  viondoa sumu ambavyo hulinda mwili dhidi sumu. Pia tafiti zinasema kwamba parachichi husaidia kulinda ini na kuzuia kansa ya mdomo.
3.       FANYA MAZOEZI YA KUTOSHA
Tafiti zinasema kwamba kukaa kwa mda mref ni sabab moja pekee inayoongeza hatari ya vifo na magonjwa, hatar ya kuugua kwa watu wasiofanya mazoezi ni sawa na hatar ya watu wanaovuta sigara. Unatakiwa kufahamu ni kwamba miili yetu iliubwa kushugulika na siyo kukaa seem moja bila movement. Weka lengo la kutembea walu hatua 7000 mpaka 10000 ambazo ni sawa na kilomita 6 mpaka 9.
4.       Kula zaidi samaki na mboga za majani
Protini ni virutubisho muhimu kwenye mwili kama sehemu ya afya na kiungo cha cell, misuli mifufa na viini vya kusaga chakula (enyzmes), lakini angalizo ulaji mwingi wa protini ni hatari kwa afya, hivo badala ya kula nyama zaidi basi kula samaki kwa wingi.
5.       Kufunga kula kwa masaa kadhaa
Moja ya mkakati ambao sio tu unaondoa kitambi na uzito mkubwa bali pia kuepusha magonjwa mengine hatari  kama kisukari matatizo ya moyo, ulaji wa kila mara ni chanzo cha matatizo haya yote na pia huufanya mwili kuana kuunguza sukari kamachanzo cha nishati badala ya mafuta kitendo ambacho hupunguza viini vinavyounguza mafuat. Tafiti zinasema kwamba mwili hujisafisha wenyewe na kujijenga vizuri  pale tumbo likiwa tupu bila chakula. Kufunga kula kunajumuisha kukaaa jumla ya masaa 13 mpaka 18 bila kula kwa siku hii unaweza kutimiza tu kwa kuvusha either chakula cha mchana ama asubuhi, na kula milo miwili tu, hivo kama utachagua kula usiku basi hakikisha unakula masaa ma3 kabla ya kulala, unapolala mwili uhuhitaji nishati kidogo na hivo unapokula chakula kingi basi mwili unazalisha sumu nyingi  kutokana na chakula kutosagw vizuri.
6.       LALA  MASAA 8 KILAUSIKU
Kutopata usngizi wa kutosha huleta madhara katika kinga ya mwili na pia kuongeza msongo wa mawazo na hatari ya kuugua maradhi. Ukosefu wa usingizi hupunguza homoni ya melatonin ambayo husaidia kukukinga dhidi ya saratani .
7.       KULA ZAIDI VYAKULA VYENYE NYUZINYUZI
Chakula chenye nyuzinyuzi kwa wingi hupunguza hatari ya vifo vya mapema kutoka kwenye ugonjwa wowte, kwa sababu husaidia kupunguza hatari ya baadhi ya magonjwa kama kisukari, magonjwa ya moyo,  na saratani. Zingatia chanzo kikubwa cha nyuzinyuzi kitoke kwenye mboga mboga, jamii za karanga na mbegu, na siyo nafaka


Comments

Popular posts from this blog

KUTOKWA NA UCHAFU UKENI, CHANZO NA TIBA YAKE

Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke. Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi. Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke. Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili. Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha. Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eno la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni. Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa. Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke. Uchafu Wa Sehemu Za Siri  Wa Kawaida Wanawake wote hutoa uchafu sehemu za siri. Kiwango cha uchafu unaotoka, ra

JINSI YA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATIZO YATOKANAYO NA KUKUA KWA TEZI DUME KWA KUTUMIA VYAKULA HIVI VI 5

Maelezo ya utangulizi. Kichocheo cha testosterone, japo huusishwa zaidi na upande wa mwananume ni muhimu kwa afya ya pande zote mbili yaani mwanamke na mwanamme pia.kadiri umri unavoenda mbele basi kiwango cha uzalishaji wa kichocheo cha testerone kupungua, kupungua kwa kichocheo hiki kunaambatana na ukuaji wa tezi dume (prostate gland),kupotea kwa nywele na pia saratani mfano saratani ya tezi dume. .KAZI KUBWA YA KICHOCHEO HIKI NI KUONGEZA MSUKUMO NA HAMU YA TENDO LA NDOA , KUIMARISHA MISULI NA MIFUPA MWILINI. NINI KINAHITAJIKA ILI KUZALISHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE? Ili kuhakikisha uzalishaji wa kichocheo cha kiume unafanyika, mwili unahitaji virutubisho au viini lishe mbalimbali, baadhi ya viini lishe hivyo ni madini ya ZINC na vitamin D3,  vitamini D inaweza kuzalishwa na mwili pale ngozi yako inapokutana na mwanga wa jua, hapa nazungumzia mwanga wa asubuhi wakati jua ndo linachomoza na pia lile jua la jion karibia na kuzama, hivyo utakubaliana na mimi kuwa wengi wet

MADHARA YA PUNYETO NA TIBA YAKE

MAELEZO  YA AWALI KUHUSU TATIZO LA UPIGAJI PUNYETO Watu wengi sana wanataka kufahamu jinsi gani wafanye ili kuachana na kitendo cha upigaji punyeto. Punyeto ni tendo la mtu la kuamsha hisia za mapenzi au msisimko ambao unampelekea mtu huyu kufikia kilele cha kujimalizia tamaa zake! Bila kufanya tendo halisi, hutumia fikra zake katika picha za zinazoitwa za ngono au picha zozote zinazoweza kulifanikisha tendo hilo, movie n.k. Kilele cha yote anafikia mahali anajimalzia tamaa zake mwenyewe!. Nimekuwa nikiona baadhi ya watu wanaosema wameelimika wakipingana wao kwa wao katika suala zima la kupiga punyeto! Wako wanaotetea kutokana na elimu yao na wanasema kwa ujasiri mkubwa kwamba "kupiga punyeto ni sehemu ya maisha ya mwanadamu" Ina maana katika maisha ya mwanadamu upigaji punyeto inaelezwa ni kama tendo la lazima mpaka inafikia mahali wanasema ni sehemu ya maisha (Maisha) ya mwanadamu. Nimekuwa nikipata kesi nyingi sana juu ya madhara yatokanayo na punyeto. Aslimia 60