Skip to main content

HATUA TANO ZA KURUDISHA NGUVU ZA KIUME KATIKA NDOA YAKO


MAELEZO YA UTANGULIZI KUHUSU UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Napenda kukukaribisha tena katika jukwaa langu la afya yako, leo hii napenda nizungumzie tatizo ambalo limekuwa ni kubwa sana kupita kiasi kwa kila mtu, tatizo ambalo linayumbisha na kuweka ndoa matatani, usiwe miongoni mwa watu wenye upungufu wa nguvu za kiume, yote hayo utayaepuka kwa kufuata ushauri huu ulio badili maisha ya watu wengi na bado elimu hii inaendelea kutoa shuhuda kwa kila mtu aliyekuwa na tatizo hili.

Tatizo la nguvu za kiume hapo zamani za kale na tafiti za kisayansi zinaonesha ni matokeo yanayotokea uzeeni, yaani  kuwa ni jambo la kawaida kwa umri mkubwa, lakini napenda nikwambie kuwa uzeeni ambao unaambatana na magonjwa sugu kiasi hicho ni moja wapo ya sababu nikuweke kwenye kundi la watu wanaozeeka vibaya. Kwa kawaida binadamu hastahili kuzeeka na magonjwa, tunazeeka na magonjwa kwa sababu tunayasababisha sisi kwa maisha ya kifahari tunayoishi na kusahau kuwa afya yako sio hazina ya milele,unatakiwa kuiheshimu,kuilinda na kuimarisha ili uje ufurahie uzee wako usio na magonjwa.
Najua kuwa hadi sasa ukifanya tafiti vijana wa umri wa miaka 20 hadi 30 ndio wanao ongoza kwa kusumbuka na matatizo haya ya nguvu za kiume tofauti na matarajio yetu wote kuwa tatizo hili tunasoma kuwa linawapata wazee, swali la kujiuliza kwa nini sasa vijana tena katika umri mdogo? Ndio maana nimeamua kukuandikia Makala hii ambapo kama ni miongoni mwa watu wanaosumbuka hili tatizo nina uhakika tatizo lako utapata suluhisho kutokana na elimu hii rafiki yangu. Pia najua unaweza ukawa na mchumba wako, unavumulia mengi kuhusu tatizo hili la mwenzi wako, usiwe mkimya kwani inahitaji utashi wa juu sana kumweleza mwenzi wako kuhusu hili swala kwani upungufu wa nguvu za kiume unasababisha msongo wa mawazo wengine hupelekea hadi kuchanganyikiwa hatimaye kupata MAJOR DEPRESSIVE DISORDER na mbali na hivyo husababisha kutokujiamini na woga wa kuwa na mke na hivyo wengi wamejaa wasiwasi na hofu kubwa ya kugunduliwa na mwezi wake kuwa ana tatizo hilo, na wengi wao ni woga sana kutogunduliwa tatizo hilo,ndio maana inapofikia hatua mwenza wako umembaini ni mara chache sana atakubali kuwa kweli ana tatizo hilo. Kwa nini usumbuke na matatizo kama haya wakati msaada wako upo?

 Usiendelee kusumbuka na tatizo hili kwani umeumbiwa maisha ya furaha na Mungu ni haki yako kufurahia uumbaji wa Mungu, anza leo kushughurikia tatizo kabla halijawa sugu mpendwa msomaji wa Makala hii.



NINI KISABABISHI MSINGI WA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME?

Katika mwili wa binadamu kuna vichocheo aina ya Testosterone ambavyo hutolewa malengo ya kuimarisha utendaji kazi wa ubongo,ufanye kazi katika hali tulivu,kuondoa msongo,kuondoa mstuko wa aina yoyote ,kuimarisha uwezo wa kufikiri,kuimarisha furaha ya mwili wako na hatimaye kuimarisha nguvu za kiume na hatimaye kufurahia tendo la ndoa. Kazi kubwa ya kichocheo hiki ni kuhakikisha mwili wako unakuwa katika hali tulivu kabisa kwa kuutuliza ubongo wako ndipo utafurahia ndoa yako rafiki yangu.

Sasa endapo kichecheo hiki kikivurugika kinasababisha vichocheo vingine kama insulin,leptin,cortisol,vichocheo vya ukuaji pia kuvurugika kwani matokeo ya hitililafu hii mwilini inasababisha  KUPUNGUKIWA NGUVU ZA KIUME kwa sababu vichocheo hivi vinafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa, na endapo kimoja tu kikivurugika vyote vinapoteza mwelekeo na tatizo kuwa sugu Zaidi.

Napenda leo nieleze kwa kina kidogo namna gani nguvu za kiume zinapotea kutokana na mvurugiko wa vichocheo hivyo vikuu vitatu kama nilivyo vitaja hapo juu.



1. TESTOSTERONE

Kichocheo hiki ndio silaha ya mwanaume kwani ndicho kichocheo ambacho kinakufanya uwe na sifa zote za kiume na ndicho kichocheo ambacho kinakufanya uwe imara katika tendo la ndoa. Upungufu wa kichocheo hiki kinasababisha kupungua kwa matamanio kwa jinsia tofauti,kupungua kwa nguvu za misuli yako kiutendaji,mafuta kurundikana ovyo mwilini( BELLY FAT AND OBESITY)

Lakini pia ijulikane kuwa kichocheo hiki cha testosterone sio kwamba kinapatikana kwa wanaume tu, la hasha! Kichocheo hiki hata wanawake wanacho ingawaje kwa kiwango cha chini sana, endapo kinapokuwa kimepungua kinaweza kumsababishia mwanamke kukosa matamanio kwa jinsia ya kiume wakati wa tendo la ndoa, kukosa nguvu ya misuli ya kuhimili tendo la ndoa (Kuchoka Sana),kuongezeka uzito kupita kiasi na nyama uzembe pia kupunguza uwezo wako katika kufikiri na kumbu kumbu.



NINI KINASHUSHA TESTOSTERONE MWILINI MWAKO?
Moja ya kisababishi kikubwa cha testosterone kushuka kiwango chake ni kwa sababu ya kuwepo na kizuizi cha insulin (insulin resistance) hii inafanya kiwango cha insulin kuwa juu sana na kusababisha testosterone kushuka kiwango chake. Moja ya sababu zinazo sababisha kiwango cha insulini kuwa juu sana ni unywaji wa vinywaji vyenye sukari nyingi kama soda na pia ulaji wa vyakula vyenye vionjo mbalimbali vitamu vilivyotengenezwa viwandani. Hivyo basi sukari inapokuwa ipo katika kiwango cha juu sana kwenye damu inasababisha utolewaji wa insulin kuwa katika kiwango cha juu pia kwenda kusawazisha sukari irudi kawaida. Hivyo basi matumizi ya vyakula na vinywaji vya sukari nyingi vinafanya mwili upate kizuizi katika utendaji kazi wa insulin na hatimaye testosterone pia kushuka kiwango chake.

Najua umejifunza sasa kwa nini watu wanaotumia vyakula vya viwandani,vinywaji vya sukari nyingi,ulaji wa vyakula vyenye mafuta mabaya jinsi gani inasababisha vichocheo vyako kushuka kiwango na unaendelea kusumbuka sana. Napenda kukuambiwa kuwa siku zote watu hawaogopi vyakula vyenye sukari wanaogopa vyakula vyenye mafuta mengi, hio ni fikra potofu sana! Sugar is more addictive than heroin and cocaine, kwa maana nyingine watu ni walevi wa vyakula na vinywaji vya sukari na haipo siku anaweza kuacha haraka. Usihofu kama una tatizo hilo ujue tayari umeshaathiriwa na ulaji wa vyakula na vinywaji hivyo.




Hiki ni kichecheo ambacho hutolewa na kongosho lako ili kwenda kusawazisha kiwango cha sukari mwilini mwako. Kazi kubwa wa maji haya ya insulin ni kuhifadhi nishati ya mwili kwa matumizi ya baadae pale mwili unapokuwa una nishati ya kutosha na hautaki kupoteza nishati ya ziada. Nishati hii huhifadhiwa asilimia kubwa  katika mfumo wa glycojeni mwilini mwako kwenye misuli,ini nk. Sasa inapotokea kiwango chako cha ulaji wa vyakula vya sukari ni kikubwa sana ndivyo kiwango kingi cha insulin kitatengenezwa na kumwagwa kwenye mzunguko wa damu kwenye kuhifadhi sukari ya ziada ambayo haitumiki wakati ule na hatimaye kusazisha kiwango cha sukari mwilini mwako. Kazi ya insulin sio kushusha sukari kama wengi tunavyofundishwa darasani! Kwa nini nasema hivi? Kazi ya insulin ni kuhifadhi nishati ya ziada kwa matumizi ya baadae na hivyo basi kupungua kwa sukari ni matokeo ya kazi ya insulin mwilini mwako. 



HEBU SOMA TAFAKURI HII:

Umeingia katika chumba ambacho umekuta harufu mbaya sana ya deodorant spray au perfume punde tu utakapo ingia katika chumba hicho utasumbuka sana na harufu hio kwa muda mfupi na hatimaye unaizoea na kuona ni harufu ambayo haina madhara wala usumbufu kwako.



Huu mfano utakusaidia kujua kwa nini tunasema insulin yako imeshindwa kufanya kazi, na umepata kizuizi katika utendaji kazi wake. Nimesema insulin hutolewa kwa kiwango kikubwa sana kulingana na kiwango cha sukari mwilini mwako, kiwango hiki kingi cha insulin kwenye damu kwa muda mrefu inaweza kupelekea insulin kupoteza kazi yake kiuhalisia. Na pia kitu kingine ambacho kinaweza kupelekea insulin kutofanya kazi ni vipokea insulin kutoitikia kwa sababu ya mafuta mabaya kuleta kizuizi katika vipokezi vya insulin. Vitendo vyote hivi viwili vinasababisha kiwango cha insulin kuwa juu wakati wote  na kama nilivyo eleza mwanzo kuwa kiwango cha insulin kinavyozidi kuwa kingi mwilini mwako kinashusha vichocheo vya Testosterone ambavyo ndio silaha yako mwanaume. Hivyo basi ukiangalia katika maelezo haya utagundua kuwa ulaji wa vyakula na vinywaji vingi vya sukari vinasababisha kiwango cha insulin kuwa juu muda wote ambapo nacho kinapelekea vichocheo vya kiume kushuka na hatimaye unakumbwa na matatizo ya kukosa matamanio kwa jinsia tofauti,msongo wa mawazo,misuli kukosa nguvu muda wote umechoka,uzito kuongezeka kwa kasi sana na wengine hupelekea kumilki vitambi.

Pia kiwango kingi cha insulin kwa muda mrefu kwenye damu kinaweza kupelekea kupata nywele usoni kwa wanawake,mwanaume kuishiwa vinyweleo sehemu kama kifuani,tumboni na maeneo mengine mengi.





3. LEPTINI

Hiki ni kichocheo cha pekee sana na huwa napenda sana kukizungumzia kwani kinaonesha jinsi gani binadamu alivyo umbwa kwa kutumia teknolojia ya uhandisi wa hali ya juu. Hiki ni kichecheo ambacho kinatengenezwa na seli zinazohifadhi mafuta ambazo zinapatikana kwa wingi kwenye misuli kazi yake kubwa ni kupeleka ujumbe kwenye ubongo katika kuendesha hamu yako unapokuwa una chakula mbele yako, na ubongo huitikia kwa kutoa taarifa ya kutosheka na chakula kwa kujihsi umeshiba na huwezi tena kuendelea na chakula.

Sasa basi ulaji wa vyakula vingi bila mpango vyenye sukari nyingi unasababisha seli za kuhifadhi mafuta (FAT CELLS) kutengeneza kwa wingi leptin ili kwenda kutimiza kazi yake. Kiwango cha insulin na leptin hupanda kwa pamoja kama mapacha vile. Hivyo hivyo kumbuka tafakari ile pale juu ya perfume, itafikia wakati kiwango kingi sana kinasababisha leptin kutokuwa na uwezo wa kufanya kazi yake ( KUKATA HAMU YA CHAKULA) hivyo utakuwa una tatizo la kula mlo mkubwa ambao hata siku moja hautosheki na ukitosheka muda si mrefu unahitaji tena kula. Hawa ndio watu wengi ni wahanga wa muda wote wanapenda kula vyakula vitamu vitamu tu, hamu haiishi (Sugary addicted,sugar craving) na wengi huishia kupata matitizo ya kiafya kama kuishiwa nguvu za kiume,uzito kupita kiasi,kitambi na kuishiwa nguvu kabisa ya misuli yote haya ni kwa sababu kiwango kingi cha leptin na insulin kinashusha vichocheo vyako vya testosterone.



4. CORTISOL 

Hiki ni kichocheo ambacho hutolewa na mwili pale unapokuwa katika hali yoyote ya mstuko ili kwenda kukabiliana na mshtuko huo.

Mfano labda mimi nilikuwa natembea njiani ghafla nikaona nyoka huyo mkubwa chatu. Mwili utastuka sana na kutoa vichecheo vinavyo enda kupambana na hio hali iliyoshtua mwili wako, mfano cortisol huenda kuongeza kiwango cha nishati ya mwili (glucose) kwenye damu na kuwa na nguvu ajabu ya kumkimbia adui yako aliyepo ,mbele yako.

Cortisol pia hutolewa hata kama mwili wako umekabiliwa na mstuko ndani kwa ndani mfano,sukari mwilini imepungua mwili unatoa cortisol ambayo kazi yake kubwa ni kubadili ile nishati iliyokuwa imehifadhiwa katika mfumo wa glycogen kwenye misuli na ini kuwa sukari na hatimaye kuongeza sukari mwilini mwako.

Sasa tafiti zinasema kwamba,kiwango kingi cha cortisol kwenye damu kinachosababishwa na msongo,mstuko ndani ya miili yetu inayo endelea inasababisha LEPTIN kutokuwa na uwezo wa kufanya kazi yake ipasavyo.

Na endapo leptin ikishindwa kufanya kazi yake ipasavyo utakuwa una tatizo la kula sana hasa vyakula na vinywaji  vya sukari bila hamu kukata na hatimaye kusababisha insulin kupanda juu na testosterone kushuka chini na hatimaye kuishiwa nguvu za kiume,matamanio kwa jinsia tofauti nk.

Hongera sana kwa kuendelea kusoma Makala hii, hapo juu nilitaka kukueleza tu nini kinatokea endapo unapatwa na upungufu wa nguvu za kiume kwani wengi mmekuwa mkinipigia simu kutaka kujua kwa nini nguvu za kiume sasa, basi leo nazani umejifunza kitu, kama hujaungana nami katika ukurasa wangu facebook hebu bofya like mkumbohealthcareproducts,

utafurahia Makala zangu nyingi sana nzuri zimeandaliwa kwa ajili yako.

Basi napenda nikupe vitu vikuu 4 vinavyo angamiza watu kukosa nguvu za kiume hawa ndio maadui wako wakuu kuhusu tatizo lako hilo mpendwa, hebu endelea kusoma upate suluhisho lako,ufurahie ndoa yako,



VITU 4 VINAVYO ANGAMIZA NGUVU ZAKO ZA KIUME NA KUKUACHA MWENYE MSONGO WA MAWAZO NA MPWEKE KATIKA MAHUSIANO AU NDOA YAKO



Hebu basi napenda nikwambie hawa maadui wako, najua utashangaa kuwa ni maadui ambao kila siku ni marafiki zako, na hujui kuwa wanaangamiza msingi wa ndoa yako na inaweza kuwa unajua lakini unayapuuzia haya tunayokufundisha kupitia elimu hii ya afya, huwa napenda kuwaambia wagonjwa wangu kuwa afya yako ni mali yako sio ya daktari wala muuguzi wewe ndiye una mamlaka ya afya yako kuiweka sawa au kuidhoofisha.  Hivyo napenda kukuambia kuwa afya yako sio hazina ya milele linda sana afya kuliko vyovyote ulindavyo kwani ndio msingi wa furaha zote duniani.





    1.      Vinywaji vyenye sukari nyingi kama soda



    Hivi ndio vimekuwa ni vinywaji vya kila siku hasa kwa wafanya kazi, ndio maana wengi ndio wamekuwa wakisumbuka na matatizo haya ya kiafya kwani wanakula vyakula huwa napenda kuviita vya chapuchapu, yani anataka soda ya kuvuta muda ili baadae akale, ndugu yangu nimeongelea jinsi gani sukari nyingi inashusha nguvu za kiume tena kwa kina Zaidi. Wengine huuliza sasa Dr mimi siwezi kabisa kujizuia kunywa soda hata masaa tu, kwani kwenye friji zimejaa, ni kweli huwezi kujizuia kwa sababu tayari umeshakuwa ni mlevi wa sukari (sugary addicted, sugary craving) vyote hivi unaweza kujizuia kwa kukutana na mshauri wa afya lishe atakupa maelekezo mazuri namna gani unaweza kukata sugar craving kiurahis kabisa. Kumbuka kiwango kimoja cha kichecheo kikivurugika vyote vinavurugika hivyo tunatakiwa kulinda sana kiwango cha insulin kuwa katika kiwango kizuri muda wote ili kufurahia ndoa zetu.

     2. Kuepuka kabisa ulaji wa vyakula vya mafuta

     

     Watu wengi sana huwa na fikra potofu kuwa chakula chochote cha mafuta ni kibaya, na hivyo hujizuia sana kula vyakula hivyo kwa kuogopa kunenepa, napenda nikwambie kuwa hakuna adui mkubwa wa magonjwa yote kama SUKARI hivyo vyakula vya sukari ndio chanzo cha magonjwa mengi ya tabia ambayo ni magonjwa sugu hapa duniani, ndio chanzo cha uzito mkubwa kupita kiasi,kitambi,shinikizo la damu,kisukari,upungufu wa nguvu za kiume,uvimbe kwenye kizazi,mzunguko mbaya wa hedhi,ugumba,utasa nk hivyo basi kuna usemi unasema “SIO MAFUTA YANAKUFANYA MGONJWA, BALI SUKARI NDIO INAKUFANYA ULEMEWE NA MAGONJWA”

   Tafiti zinaonesha kuwa ulaji wa vyakula yenye mafuta kidogo sana tafiti zinaonesha kuwa vichocheo vya progesterone hupungua na kupelekea kupoteza nguvu za kiume na matamanio kwa jinsia tofauti. 



   3. Vyakula vyote vya kusindika viwandani

   Napenda kusema kuwa ulaji wa vyakula hivi sio ufahali katika familia yako, bali ni uzembe katika uandaaji chakula katika familia yako, kuna usemi unasema kuwa, ukitaka uishi kwa bajeti kubwa katika familia yako, kula vyakula asili ambavyo babu zetu walikula enzi zile (EAT ORGANIC) ndio maana watu wengi hawapendi kula vyakula asili, wanatafuta vyakula vilivyo sindikwa kwani havina gharama kubwa. Kuna usemi unasema, unapokuwa upo jikoni unandaa chakula chako kwa familia yako, unatakiwa ujiulize kwa nini vyakula hivi vya kusindika vina bei rahisi kiasi  hiki?

   Ulaji wa vyakula hivi,siku zote huenda kuangamiza bakteria rafiki (Normal flora) pia wengi hupendelea kuita gut probiotics na unapokuwa umewaangamiza hawa ndio chanzo cha magonjwa yote kwani katika Makala zangu zilizopita nilieleza namna gani mfumo wa chakula unaweza kuwa chanzo cha afya bora yako, na chanzo cha magonjwa yote mwilini mwako. Unapokuwa umeangamiza hawa viumbe katika mfumo wa chakula kwa sababu ya vyakula ambavyo wao, hawavitambui, unakuwa ni mtu wakushambuliwa na maradhi nyemelezi yote na kudhoofisha ukuta wa mfumo wa chakula na hatimaye unaweza kuanza kupenyeza sumu (toxins), bakteria wabaya kama E. Coli, vyakula ambavyo havijameng’enywa vizuri na protini zingine kama gluten ambazo ni hatari kwa afya yako. Hivyo kama wewe umekuwa ukisumbuka na nguvu za kiume na umekuwa ni mlaji mzuri sana wa vyakula hivyo, hakikisha una viepuka kuwa mtu unayependa vyakula asili, vitarudisha uhalisia wa mfumo wako wako wa chakula kwa kuondoa tatizo la tumbo kujaa gesi na choo kuwa ngumu.


   4. Sumu mbali mbali kutoka kwenye mazingira
   Watu wengi sana wanapokuwa wanazungumzia tatizo la nguvu za kiume wanasahau kuahusisha mahusiano yaliyopo kati ya upungufu wa nguvu za kiume na mazingira yako. Najua kuwa tumekuwa tukijishughurisha na shughuli mbali mbali ambazo zinatufanya tugusane na sumu mbali mbali, mfano madini ya mercury ambayo sasa yapo kila kona katika biashara zetu, madini ya lead haya ni madini mazito na hatari sana kwenye kudhoofisha utendaji kazi wa mwili wako, kukuletea msongo wa muda mefu na mengine mengi ambayo yanapelekea kupoteza nguvu za kiume. Kwa dunia ya sasa ya viwanda huwezi kuziepuka sumu kama hizi mwilini mwako, ni jukumu lako kuhakikisha unajijengea mazoea ya kuondoa sum nzito hizi na mionzi mbali mbali katika mwili wako na hatimaye kuimarisha afya yako.

   Najua umejifunza kwa nini sasa una upungufu wa nguvu za kiume au huna kabisa nguvu za kiume basi ningependa ijifunze jinsi gani unaweza kuhakikisha unaondokana na tatizo hili na ukafurahia ndoa yako na mahusiano yako kuanzia sasa, naomba basi nikuokoe katika tatizo hilo kwa kusoma njia tano za kurudisha nguvu za kiume.


   NJIA TANO ZA KURUDISHA NGUVU ZA KIUME 

  Najua umekuwa ukisumbuka kila siku kufurahia ndoa yako, hadi imefikia hatua mbaya, najua umekuwa mnyonge na mwoga wa kugundulika kwa mwenza wako kuwa unasumbuka na tatizo hilo, umejaa woga, umegubikwa na msongo wa mawazo na umekuwa ukizunguka kila sehemu upate msaada na hatimaye umekuwa ukitoa pesa bila hata kurudisha furaha ya ndoa yako na nafsi yako! Pole lakini elimu ni bora kuliko yote yaliyokupata ndugu, hebu soma hiki ambacho nimekuwa nikipewa asante kila siku na wagonjwa wangu wewe pia uwe miongoni mwao.

   1. Epuka vinywaji vyote vyenye sukari nyingi,vya kusindika, vyenye vionjo vya sukari,rangi na radha katika afya yako kwani vyakula hivyo ni adui mkubwa sana wa afya yako hasa wakati unataka kurudisha nguvu za kiume. Kula vyakula asili, nafaka ambayo haijakobolewa,matunda kwa wingi ambayo hayasagwa yenye nyuzi nyuzi nyingi na pia juice ya matunda na mboga za majani. Utafurahia maisha ya kula vyakula asili na utafurahia ndoa yako. Anza kuanzia leo rafiki 
   2. Epuka pombe katika maisha yako yote kwani tafiti zinaonesha kwamba pombe inakupa hamu au shauku ya kufanya tendo la ndoa lakini inakunyima uwezo wa kufanya tendo la ndoa! Najua utashangaa lakini ndivyo ilivyo, kuna usemi wa kiingeleza unasema,  “It provokes the desire, but it takes away the performance,”  sio hayo tu mpendwa pombe pia sugu, ni chanzo cha msongo wa mawazo  na kukupelekea kukosa kabisa hamu ya tendo la ndoa
    3. Fanya mazoezi ya kutosha. Watu wengi wamelemewa na magonjwa kwa sababu tu mwili haupati damu ya kutosha kwenda sehemu mbali mbali kama vile ubongo,ini,figo ambazo ndio sehemu zenye kuufanya mwili wako ufanye kazi katika uhalisia wake. Hivyo basi magonjwa mengi ya msunguko wa damu ni pamoja na nguvu za kiume kwani kama hufanyi mazoezi mwili wako unadhofika na kukosa uwezo wa kuhimili ndoa yako pia inapunguza nguvu za kiume. Basi ningependa kuwa kwa wale wazee siku hizi kuna vituo mbalimbali ambavyo vitakusaidia mwili wako kuwa imara na kurudisha uwezo wako katika tendo la ndoa kupitia mazoezi. Unaweza pia kuwasiliana nami nitakupa taratibu za kufuata kukusaidia uanze mazoezi ya viungo kwa kutumia mashine maalumu kwa umri wako ambazo zitasaidia kuimarisha mwili wako. Mazoezi huimarisha mwili wako na kuweka mbali mwili wako na maradhi mbalimbali yanayo sababishwa na uzembe.
    4. Rudisha Virutubisho ambavyo vimepotea mwilini mwako
   Hakikisha mwili wako unaupa madini ya msingi kama zinki,chuma, selenium, manganese na vitamin nyingi, kwani madini haya ndiyo yanafanya mwili wako ufanye kazi katika kiwango stahiki kwani huwezesha viendesha shughuli za mwili yani enzymes kufanya kazi katika kiwango kizuri na kuimarisha mwili wako.
  Unaweza kupata madini haya yote kutoka kwenye mboga za majani kama wewe ni mvivu basi unaweza kunywa juice inayotokana na mboga mboga kama kabeji,spinachi kale, nk. Kwa wale ambao ni kazi sana kuhimili zoezi hilo unaweza kujipatia kirutubisho hicho ofsini kwetu ambacho kina madini yote hayo.
    5. Ondoa mafuta mabaya ambayo yanapunguza utendaji kazi wa mzunguko wa damu, unaweza kuondoa kolestero mbaya mwilini mwako kwa kutumia mafuta ya omega 3 ambayo unaweza kula vyakula vyenye mafuta haya kama samaki kwa wingi, flaxseeds, blackseeds ni baadhi ya vyakula ambavyo vimekuwa vikionekana kwenye nukuu za habari kuwa ni vyakula vyenye uwezo mkubwa wa kusafisha mafuta mabaya  mwilini mwako. Unaweza pia kufika ofsini kwetu kama utahitaji mafuta haya yaliyotengenezwa kitalamu utayapata na yatakusaidia.
   6. Ondoa Sumu kwa kutumia viondoa sumu. Kuna sumu aina kuu tatu ambazo mimi huwa napenda kuziongelea siku zote na kushughurika nazo kwa wagonjwa wangu kama zifuatazo,
        -Sumu ambayo inatokana na mabaki ya hewa ya oksijeni yani Free radicals ambayo ni moja wapo inaweza kuumiza seli za mwili wako na kusababisha seli zako kubadili mtazamo wa ukuaji na kuendelea kuzalishwa seli mbovu na hatimaye zinaweza kupelekea hata kupata kansa.
      -Sumu ambazo tunazipata kutoka katika mazingira yetu ya kazi kwa kukutana na metali nzito kama lead, na mercury ambazo ni kizuizi kikubwa sana katika utendaji wa mwili wako, pia sumu inayotokana na mionzi mbalimbali inayotokana na kuchokozwa kwa miamba ya ardhi ( Earth’s crust)
       -Sumu inayotokana na vyakula tunavyokula ambavyo huenda na kuathiri mfumo wako wa chakula na hatimaye kuharibu ulizi wa mwili wako katika mfumo wa chakula. Afya yako huanzia katika mfumo wa chakula na magonjwa yote huanzia katika mfumo wa chakula.


    kupitia ofisi zetu za Dar es salaam hapa Upanga -Tunakupatiapackage ya siku 30 ambayo napenda kuitambulisha kwako kama SEX DRIVE ENHANCING PACKAGE kwa gharama ya sh 150,000/= ambayo itakuondolea sumu zote za free radicals na metali nzito za aina zote na kurudisha utendaji kazi wa mwili wako na kurudisha nguvu za kiume.virytubisho na dawa zetu ni za asili zipo katika mfumo wa vidonge/capsules.


-   Kwa wale ambao umri kidogo umeenda hawawezi kufanya mazoezi vizuri ningependa ufike ofsini kwetu tuje tukusaidie tatizo lako.

   Najua umejifunza mengi sana kuhusu tatizo la nguvu za kiume, sasa napenda nihitimishe kwa kukuambia kuwa suluhisho la nguvu za kiume lipo kabisa ni kuhakikisha tu, unaliondoa tatizo hilo kwa kufuata elimu hii, na kama unaona elimu hii ni muhimu kwako basi unaweza pia kutupigia na kufika ofsini kwetu moja kwa moja kupata suluhisho la tatizo lako.
Kwa maoni na ushauri ama unahitaji tiba zetu.
Tupigie kwa namba 

0714206306


Pia waweza share makala hii ili iweze kuwafikia wahanga wengi wa matatzo haya ya kiafya. 


Usiache kufatilia makala yetu inayofuata: Madhara ya upigaji punyeto



Comments

Popular posts from this blog

KUTOKWA NA UCHAFU UKENI, CHANZO NA TIBA YAKE

Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke. Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi. Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke. Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili. Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha. Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eno la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni. Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa. Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke. Uchafu Wa Sehemu Za Siri  Wa Kawaida Wanawake wote hutoa uchafu sehemu za siri. Kiwango cha uchafu unaotoka, ra

JINSI YA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATIZO YATOKANAYO NA KUKUA KWA TEZI DUME KWA KUTUMIA VYAKULA HIVI VI 5

Maelezo ya utangulizi. Kichocheo cha testosterone, japo huusishwa zaidi na upande wa mwananume ni muhimu kwa afya ya pande zote mbili yaani mwanamke na mwanamme pia.kadiri umri unavoenda mbele basi kiwango cha uzalishaji wa kichocheo cha testerone kupungua, kupungua kwa kichocheo hiki kunaambatana na ukuaji wa tezi dume (prostate gland),kupotea kwa nywele na pia saratani mfano saratani ya tezi dume. .KAZI KUBWA YA KICHOCHEO HIKI NI KUONGEZA MSUKUMO NA HAMU YA TENDO LA NDOA , KUIMARISHA MISULI NA MIFUPA MWILINI. NINI KINAHITAJIKA ILI KUZALISHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE? Ili kuhakikisha uzalishaji wa kichocheo cha kiume unafanyika, mwili unahitaji virutubisho au viini lishe mbalimbali, baadhi ya viini lishe hivyo ni madini ya ZINC na vitamin D3,  vitamini D inaweza kuzalishwa na mwili pale ngozi yako inapokutana na mwanga wa jua, hapa nazungumzia mwanga wa asubuhi wakati jua ndo linachomoza na pia lile jua la jion karibia na kuzama, hivyo utakubaliana na mimi kuwa wengi wet

MADHARA YA PUNYETO NA TIBA YAKE

MAELEZO  YA AWALI KUHUSU TATIZO LA UPIGAJI PUNYETO Watu wengi sana wanataka kufahamu jinsi gani wafanye ili kuachana na kitendo cha upigaji punyeto. Punyeto ni tendo la mtu la kuamsha hisia za mapenzi au msisimko ambao unampelekea mtu huyu kufikia kilele cha kujimalizia tamaa zake! Bila kufanya tendo halisi, hutumia fikra zake katika picha za zinazoitwa za ngono au picha zozote zinazoweza kulifanikisha tendo hilo, movie n.k. Kilele cha yote anafikia mahali anajimalzia tamaa zake mwenyewe!. Nimekuwa nikiona baadhi ya watu wanaosema wameelimika wakipingana wao kwa wao katika suala zima la kupiga punyeto! Wako wanaotetea kutokana na elimu yao na wanasema kwa ujasiri mkubwa kwamba "kupiga punyeto ni sehemu ya maisha ya mwanadamu" Ina maana katika maisha ya mwanadamu upigaji punyeto inaelezwa ni kama tendo la lazima mpaka inafikia mahali wanasema ni sehemu ya maisha (Maisha) ya mwanadamu. Nimekuwa nikipata kesi nyingi sana juu ya madhara yatokanayo na punyeto. Aslimia 60