Skip to main content

NAMNA YA KUTUMIA TUNDA LA TOFAHA (APPLE ) KATIKA KUPUNGUZA KITAMBI/UZITO MKUBWA NA KUBORESHA KINGA YA MWILI WAKO


Leo napenda tuangalie kuusu manufaa ya tunda hili ambalo linapendwa sana na watu na pia lina gharama sana kununua hapa kwetu, kutokana tu na upekee wake

1.      Tunda hili ni miongoni mwa matunda yenye vitamin nyingi sana na viondoa sumu mwilini (ant oxidants) na mbali zaidi apple ni miongoni mwa tunda tunaloshauriwa kula na maganda yake kwani viondoa sumu hivi na vitamini vingi vinapatikana na ganda la tunda hili la apple.
Unapotaka kuwa mlaji mzuri wa tunda hili hakikisha unachagua tunda ambalo una uhakika limelimwa kienyeji kabisa kwani tunda hili ni miongoni mwa matunda yanayo ongoza duniani kwa kumwagiwa dawa za viua watududu na kemikali mbali mbali. Na kumbuka dawa nyingi za viua wadudu ni LIPOPHILIC (Ni marafiki na mafuta yapatikanayo kwenye tunda) hivyo basi dawa za wadudu huwa zinapenya ganda la matunda haya na kuingia ndani haraka sana hivyo unakiwa kuwa makini na kuhakikisha tunda lako ni asili kabisa (organic).
CHAGUA APPLE ZENYE SIFA HIZI
·         Haina kabisa kemikal
·         Apple yenye mng'ao mzuri asili sio yenye rangi iliyofifia(Dull color)
·         Chakua apple ambayo haina michubuko yoyote,shimo  na ngumu (firm)
Nina imani utafurahia utafurahia ulaji wa tunda hili kwani ni tunda ambalo limeonesha kukulinda dhidi ya maradhi mbali mbali nitakayo kwenda kuelezea.

2.      Tunda la apple ni miongoni mwa matunda ambayo yana nyuzi (fiber) nyingi sana ndani yake.
Basi kwa sababu hio napenda nikwambie kuwa aina ya fiber ipatikanayo katika tunda hili ni adimu.

KAZI YA FIBERS(NYUZI) KATIKA MIILI YETU
i. Inafanya shughuri za umeng'enyaji chakula kufanyika katika kiwango kinachostahili.
Unapokula fibers kwa wingi zinakusaidia mfumo wa umeng'enyaji chakula kufanyika polepole na hivyo hii hali itakufanya ukae muda mrefu ukiwa huna njaa kabisa tumbo limejaa.
Hivyo kwa wale wanaopenda kupunguza uzito, na wale ambao ni sugar addicted (walevi wa vyakula na vinywaji vya sukari) basi tunda hili linaweza kukata kabisa tatizo hilo na kufurahia. Watu wengi wanaotumia tunda hili sambamba na mlo wao huwasaidia sana kupunguza ulaji sana na kuwafanya muda wote wameshiba na kuwasaidia kupunguza uzito kiasi na kumaintain miili yao.

ii. Vyakula vya fibers (nyuzi) husaidia kuondoa sumu mbali mbali za vyakula mfano lead na mercury kwenye kuta za utumbo wa chakula na kukuzuia kupata magonjwa kama kansa ya utumbo mpana na mengineyo.

ii.Pia tunda hili linasaidia kuondoa constipation (choo kigumu) na kukuepusha kupata magonjwa ya mfumo wa chakula kama bawasili (vinyama sehemu za siri) kutokana na constipation ya muda mrefu.

Hivyo furahia aina hii ya fiber yani pectin katika tunda hili la apple utakuwa umejiepusha na magonjwa yafutayo
~Uzito mkubwa kupita kiasi
~Kitambi na magonjwa ya moyo
~Kiharusi yani stroke
~Bawasiri
~Mzunguko mbaya wa hedhi
~Ulevi wa vinywaji na vyakula vyenye sukari na vionjo vya kemikali
~Kisukari


3. Apple ni tunda ambalo lina aina ya sukari ambayo hutumika kuzalisha nishati ya mwili ambayo inaitwa FRUCTOSE.
Kutokana na tafiti mbali mbali hapa duniani aina hii ya sukari imeonesha kuwa chanzo kikubwa kinacho sababidha UZITO MKUBWA KUPITA KIASI, MAGONJWA YA MOYO, KISUKARI nk hivyo basi tunda hili linatakiwa liliwe katika kiwango ambacho sio hatari kwa afya yetu. Ulaji wa tunda hili bila mpangilio ni kisababishi kikubwa cha uzito mkubwa, insulini(kichocheo kinasawazisha sukari mwilini) kutofanya kazi, na kisukari cha ukubwani.
KUTOKANA NA KIWANGO KINGI CHA AINA HII YA SUKARI AMBAYO IMEKUWA NI HATARI KWA AFYA YETU AMBAYO INAKADIRIWA KUWA NI GRAMU 9.5 KWA APPLE LENYE UMBO SAIZI YA KATI.

NOTE: KAMA WEWE NI MGONJWA WA KISUKARI, UZITO MKUBWA, UNA BELLY FATS (NYAMA UZEMBE AMBAZO NI ISHARI INSULINI IMEANZA KUPATA KIPINGAMIZI KWENYE UTENDAJI)

Nakunashauri kwa siku moja kiwango cha tunda hili usizidishe gramu 15 kwa siku ambayo ni sawa APPLE MOJA NA KIGANJA CHA ZABIBU (Kumbuka apple na zabibu yote ni matunda yenye chachu unaweza kula katika mlo mmoja)

LAKINI KAMA WEWE NI MZIMA MWENYE AFYA NJEMA  yani hauna kisukari, huna uzito mkubwa, huna nyama uzembe (belly fats) ,huna mafuta mabaya kwenye moyo na mishipa ya damu (bad cholesteral)
Nakushauri kuwa unaweza kula mpaka apple 2-4 kwa siku lakini hakikisha UNAFANYA MAZOEZI YAKUTOSHA AU KUJIHUSISHA NA SHUGHURI NGUMU ZA KIMAISHA. UKIFANYA HIVYO HUWEZI KUPATA MARADHI YASABABISHWAYO NA AINA HII YA SUKARI NDANI YA TUNDA LA APPLE.

Nina IMANI KUBWA UMEJIFUNZA NAMNA GANI UNAWEZA KUANDAA TUNDA LAKO KIKUBWA NI KUZINGATIA KUWA MATUNDA MAZURI NI ORGANIC.

Hakikisha UNAFUATA SHERIA KUU SABA ZA UOASHAJI WA MATUNDA KULINGANA NA MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA
1. Osha mikono yako kwa sekunde 20 kwa maji ya uvugu vugu na sabuni kabla ya kuandaa tunda lako.
2. Ondoa kipande chochote ambacho kimeharibika kwenye tunda lako
3. Osha kwa kusafisha kwa nguvu kwa kutumia maji yanayo safisi (tape water) au maji yanayotiririka.
4. Osha tunda lako vizuri kabla ya kumenya /kula kwa kutumia maji yanayotiririka
5. Kama ni matunda /mboga tumia brashi maalumu safi yenye kuondoa wadudu na kemikali mbali mbali.
6. Chukua kitambaa chako SAFI KAUSHA MATUNDA YAKO.
7. KAMA NI MBOGA KAMA KABEJI TUPA MAGANDA YA NJE NA UBAKIZE YA NDANI( Hupunguza kiwango cha kemikali, wadudu na madawa mbali mbali)

NOTE: KUMBUKA NJIA HIZO ZIMETOLEWA NA MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA DUNIANI, ZINASAIDIA KUPUNGUZA DAWA ZILIZOPULIZIWA KWENYE MATUNDA, ZINASAIDIA KUONDOA WADUDU (VIMELEA) NA KUKUFANYA ULE TUNDA LAKO SALAMA.

Imeandaliwa na
Elphas Mkumbo
Inapatikana pia moja kwa moja kupitia page  yetu ya afya kwenye facebook
mkumbohealthcareproducts.

Kwa maoni na ushauri tuandikie kwa email. elifasimkumbo@gmail.com
Pia whatsap  0678626254, usisahau kushare Makala hii na marafiki zako ili tuzidi kuelimishana..

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUGUNDUA NA KUTHIBITI VIDONDA VYA TUMBO( PEPTIC ULCER)

MAELEZO YA UTANGULIZI KUHUSU VIDONDA VYA TUMBO Tunashukuru kwa kuendelea kufatilia makala zetu, kwa maoni na ushauri ama uhitaji wa kufika ofisini basi endelea kutuandikia kwa namba  0714206306 .  Kupata ufahamu mpana juu ya vidonda vya tumbo ni vema kuelewa kwanza mfumo unaohusika na tumbo ambao ni umen'genyaji wa chakula. Sehemu kuu zinazohusika katika umen'genyaji huo ni kinywa,umio ambayo ni misuli wenye urefu wa sentimeta 23 ambao huunganisha koromeo na tumbo'esophagus',mfuko wa nyongo na sehemu ya mwanzo ya utumbo mdogo'duodenum',utumbo mdogo,kongosho,utumbo mpana na sehemu ya mwish oni ya utumbo'rectum'. Mfumo wa mmen'genyo wa chakula hasa kuta za umio,tumbo na utumbo mwembamba hupata mmomonyoko ambao husababishwa na tindikali inayotumika kumen'genya chakula inaposhambulia kuta hizo, hii ndiyo vidonda vya tumbo'Peptic Ulcers',vidonda vya mfumo wa umen'genyaji chakula vikiwa kwenye tumbo ni 'Gastric Ulcer'vikiwa kati...

Kisonono ni nini ?, je kuna Tiba ya kisonono ?

Nini maana ya kisonono, je naweza kupata tiba sahihi ya kisonono?  Soma makala jii upate kujifunza na kupata ueewa juu ya tatizo la kisonono ambalo limeathiri watu wengi sana kwa sasa hasa vijana wa kiume. Kisonono au kwa lugha ya kitaalamu Gonorrhea ni moja ya ugonjwa wa ngono ambao huambukizwa baada ya mtu mmoja mwenye ugonjwa kukutana kimwili mtu mwingine mzima. Kisonono mara nyingi husababisha maumivu makali na dalili zingine mbaya kwenye via vya uzazi na sehemu zingine kama, sehemu ya haja kubwa, macho na pia maumivu ya viungo. Ugonjwa huu wa kisonono huweza kuwapata watu wa jinsia zote wanawake kwa wanaume huku tafiti zikionesha kwamba wanaume ndio wanaoongoza kuambukizwa kuliko wanawake. Nnini husababisha kinonono au Gonorrhea?? Ugonjwa huu wakuambukizwa kwa njia ya ngono husababishwa na bacteria wanaoitwa Neisseria gonorrhoeae. Na hivo pale watu wanapokutana kingono bacteria hawa huweza kusambaa kwenda kwa mtu mwingine kutokana na msuguano wa viungo laini vya uza...

UVIMBE KATIKA MAYAI YA MWANAMKE

 FAHAMU TATIZO LA UVIMBE KATIKA MAYAI YA MWANAMKE (OVARIAN CYST ) Uvimbe kwenye mayai ya mwanamke (ovary) hutokana na mkusanyiko wa majimaji yanayozungukwa na kuta nyembamba ndani ya mayai ya mwanamke. Uvimbe huu ambao hupatikana ndani ya mayai ya mwanamke ndio unaojulikana kama ovarian cyst. Uvimbe huu unaweza kumtokea mwanamke wa umri wowote ingawa mara nyingi huonekana kwa wanawake waliofikia kikomo cha umri wa kupata ujauzito. MAYAI YA MWANAMKE  Kwa kawaida mwanamke anakuwa na mayai mawili katika mwili wake. Yai moja upande wa kulia na yai jingine upande wa kushoto. Mayai haya hupatikana pembezoni mwa mfuko wa uzazi (uterus). Mayai haya huanza kuzalisha mayai ya uzazi yanayojulikana kama ovum  ambapo mayai hayo ya uzazi hukuwa ndani ya mayai ya mwanamke (ovary) kwa kuchochewa na baadhi ya homoni.  Katikati ya mwezi, siku ya kumi na nne, saa 24-36 baada ya kiwango cha kichocheo aina ya Luteinizing Hormone kuwa juu, mayai ya uzazi hutolewa k...