Skip to main content

KUTOKWA NA UCHAFU UKENI, CHANZO NA TIBA YAKE

Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke. Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi. Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke.

Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili. Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha. Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eno la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni.

Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa. Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke.

  1. Uchafu Wa Sehemu Za Siri  Wa Kawaida

Wanawake wote hutoa uchafu sehemu za siri. Kiwango cha uchafu unaotoka, rangi yake na harufu yake vitabalikabadilika kutoka kipindi kimoja hadi kingine kulingana na muda mwanamke aliopo katika mzunguko wake wa mwezi. Uchafu huu utabadilika vilevile kama ananyonyesha, atakuwa na hisia za kufanya mapenzi, atakuwa na mabadiliko ya lishe, anatumia madawa hasa ya mpango wa uzazi au atakuwa na ujauzito. 
Kwa kawaida uchafu huu huwa usio na rangi, wenye rangi yenye weupe wa mawingu au njanonjano pale unapokaukia kwenye nguo. Unaweza kuwa na vijipande vidogovidogo na mara nyingine ukawa wa kunatanata.

             2. Uchafu Wa Ukeni Usio Wa Kawaida

Madiliko ya uwingi wa uchafu unaotoka au katika rangi ya uchafu unaotoka ni dalili ya maambukizi ya magonjwa katika uke. Maambukizi katika uke ni tatizo la kawaida kwa wanawake na wanawake wengi wameshapata tatizo la maambukizi angalau mara moja katika maisha yao. Ukiona yafuatayo, ujue unaweza kuwa na tatizo la maambukizi ya vijijidudu vya maradhi katika uke wako:
  •  Kutokwa na uchafu ukeni kunakoambatana na kuwashwa au vijipele
  • Kutokwa na uchafu ukeni ambako ni endelevu na kwa kiwango kinachozidi kila siku
  • Kusikia maumivu wakati wa kutoa haja ndogo Kutokwa na uchafu mweupe, mzito kama jibini
  • Uchafu wa kijivu/mweupe au njano/kijani unaotoa harufu mbaya

Aina Za Uchafu Wa Ukeni Usio Wa Kawaida

Kitu chochote kitakachoharibu uwiano wa bakteria wa kawaida waishio katika uke kinaweza kuleta mabadiliko katika rangi, harufu au muundo wa uchafu utakaotoka katika uke. Hapa chini naonyesha aina ya uchafu unaotoka, maana yake au chazo chake na dalili ambazo zitatokea kwenye mwili wa mwanamke husika:

  • Uchafu Wenye Damu Au Wa Rangi Ya Kahawia.

Hii ni dalili ya mzungumko wa mwezi wa mwanamke uliovurugika na mara chache ni dalili ya kansa ya Cervix au aina nyingine ya kansa iitwayo endometrial cancer. Mwanamke mwenye tatizo hili atatoa damu nyingi ukeni na kuumwa nyonga.
  • Uchafu Wenye Rangi Ya Mawingu Au Njano

Hii ni dalili ya ugonjwa wa kisonono (Gonorrhea). Mwanamke atatokwa na damu katikati ya siku zake, atatokwa na mkojo bila kukusudia na kupata maumivu ya nyonga.
  • Uchafu Wa Njano Au Kijani Wenye Harufu Mbaya

Endapo uchafu utatoka kama mapovu, wenye rangi ya kijani au njano ukiambatana na harufu mbaya , hii ni dalili ya Trichomoniasis, maambukizi (parasitic) yanayotokana na ngono zembe. Dalili nyigine ni maumivu na kuwashwa wakati wa kutoa haja ndogo.

  • Uchafu Mweupe Mzito Kama Jibini

Hii ni dalili ya maambukizi ya aina ya fungus (Yeast infection) na dalili nyingine atakazozisikia mwanamke huyu ni kuvimba na maumivu kwenye sehemu za nje za siri (vulva), kuwashwa na maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa.
  • Uchafu Mweupe, Wa Njano Au Wa Kijivu Wenye Harufu Ya Samaki

 Uchafu wa aina hii ni dalili za maabukizi ya Bacterial Vaginosis. Mwanamke mwenye tatizo hili atasikia miwasho au maumivu, kuvimba kwa uke au sehemu ya nje ya uke (vulva).


 Aina Ya Maambukizi Ya Ukeni

Kuifanya mada yetu iwe na maana na msaada zaidi, tutazungumzia kwa undani zaidi aina tatu za maambukizi ya ukeni ambazo zinawasumbua wanawake wengi zaidi, ambapo tutatazama dalili zake na kuelezea tiba ambazo zinawea kutolewa kuondoa matatizo hayo. Hapa tutazungumzia Bacterial Vaginosis, Trichomoniasis na Monilia (Yeast) Infection.
Bacterial Vaginosis: Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakifahamiki. Kinachotokea ni kuongezeka kwa ghafla kwa idadi ya bacteria hawa na kubadilisha uwiano wake kwenye mazingira ya uke. Wanawake wenye wapenzi wengi au wanaofanya mapenzi kupitia midomo wanakuwa kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata maambukizi ya Bacterial Vaginosis.
Dalili za Bacterial Vaginosis:

– Kuongezeka kwa uchafu unaotoka ukeni

– Kutokwa na uchafu wa kijivu/mweupe, mwepesi au wa majimaji

– Harufu kama ya samaki ikiambatana na uchafu

– Harufu inayozidi au uchafu unaozidi mara baada ya kufanya tendo la ndoa.

Tiba kwa tatizo la bacterial vaginosis zipo za aina mbili. Tiba ya aina ya kwanza ni kutumia  metronidazole (Flagyl) na tiba ya pili ni kutumia antibiotic ya vidonge au ya cream.
Trichomoniasis: Maambukizi haya hutokana na aina ya protozoa wa seli moja. Trichomoniasis maranyingi huambukizwa kwa kufanya ngono. Protozoa huyu huweza kukaa kwenye mazingira ya unyevunyevu kwa muda wa saa 24 bila kufa hivyo kufanya taulo na nguo nyingine za kuogea kuwa chanzo kingine kikuu cha maambukizi.

Dalili Za Trichomoniasis

– Kutokwa na uchafu wa rangi ya njano/kijani ulio kama mapovu

– Harufu mbaya inayoambatana na kutokwa na uchafu

– Kuongezeka kwa uwingi wa uchafu wa ukeni

– Maumivu ya ukeni au sehemu za nje ya uke (vulva)

– Kujisaidia haja ndogo mara nyingi zaidi

– Kuwashwa sehemu za siri

Tiba ya Trichomoniasis ni kunywa vidonge vya antibiotic, metronidazole.

Monilia (Yeast) Infection: Kwa kawaida kuna kiwango kidogo cha yeast (Candida albicans) katika uke. Tunasema kuna maambukizi ya yeast pale kiwango chao kinapozidi hali ambayo inatokana na kubadilika kwa hali ya ukeni (change in the pH balance of the vagina). Maambukizi ya yeast hayatokani na tendo la ngono. Kuna mambo ambayo yanaweza kusababisha kuongezeka kwa yeast katika uke, nayo ni; msongo wa mawazo, matumizi ya dawa za kuziua mimba,kisukari, ujauzito na matumizi ya antibotics.


Dalili Za Monilia (Yeast) Infection


– Mwongezeko wa uchafu unaotoka ukeni

– Uchafu mweupe unaotoka katika vifungu vidogo kama vya jibini

– Kuwashwa na mauvivu ya ukeni au sehemu za nje (vulva)

Tiba ya Monilia (Yeast) Infection inalenga kuzuia mwongezeko wa yeast katika uke na kuwarudisha kwenye kiwango kinachofaa na si kuwaondoa. Tiba ni kutumia vidonge vya antifungal na cream za kupaka ukeni. Kuna dawa nyingi za kuweza kuondoa tatizo hili.
 USHAURI.
unapoona dalili hatari kama tulivoelelezea hapo juu basi fika haraka hospitali kupata vipimo na ushauri wa dactari. kama tatizo limekuwa sugu na umetumia dawa nyingi bila msaada basi usikate tamaa, unaweza kufika ofsini kwetu Mwembechai ukapata huduma ya dawa kupitimia vodonge vya mimea na ushauri ili kutibu tatizo lako.
tuandikie mda wowote.
Hakikisha tu umefanya vipimo na kujua chanzo cha tatizo lako.

Tiba yetu inagarimu Tsh 50,000/= elfu hamsini tu

Chati na Daktari Whatsapp kwa namba 0678626254 uanze tiba

Soma Makala inayofuata : Harufu mbaya ukeni husababishwa na nini



Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATIZO YATOKANAYO NA KUKUA KWA TEZI DUME KWA KUTUMIA VYAKULA HIVI VI 5

Maelezo ya utangulizi. Kichocheo cha testosterone, japo huusishwa zaidi na upande wa mwananume ni muhimu kwa afya ya pande zote mbili yaani mwanamke na mwanamme pia.kadiri umri unavoenda mbele basi kiwango cha uzalishaji wa kichocheo cha testerone kupungua, kupungua kwa kichocheo hiki kunaambatana na ukuaji wa tezi dume (prostate gland),kupotea kwa nywele na pia saratani mfano saratani ya tezi dume. .KAZI KUBWA YA KICHOCHEO HIKI NI KUONGEZA MSUKUMO NA HAMU YA TENDO LA NDOA , KUIMARISHA MISULI NA MIFUPA MWILINI. NINI KINAHITAJIKA ILI KUZALISHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE? Ili kuhakikisha uzalishaji wa kichocheo cha kiume unafanyika, mwili unahitaji virutubisho au viini lishe mbalimbali, baadhi ya viini lishe hivyo ni madini ya ZINC na vitamin D3,  vitamini D inaweza kuzalishwa na mwili pale ngozi yako inapokutana na mwanga wa jua, hapa nazungumzia mwanga wa asubuhi wakati jua ndo linachomoza na pia lile jua la jion karibia na kuzama, hivyo utakubaliana na mimi kuwa wengi wet

MADHARA YA PUNYETO NA TIBA YAKE

MAELEZO  YA AWALI KUHUSU TATIZO LA UPIGAJI PUNYETO Watu wengi sana wanataka kufahamu jinsi gani wafanye ili kuachana na kitendo cha upigaji punyeto. Punyeto ni tendo la mtu la kuamsha hisia za mapenzi au msisimko ambao unampelekea mtu huyu kufikia kilele cha kujimalizia tamaa zake! Bila kufanya tendo halisi, hutumia fikra zake katika picha za zinazoitwa za ngono au picha zozote zinazoweza kulifanikisha tendo hilo, movie n.k. Kilele cha yote anafikia mahali anajimalzia tamaa zake mwenyewe!. Nimekuwa nikiona baadhi ya watu wanaosema wameelimika wakipingana wao kwa wao katika suala zima la kupiga punyeto! Wako wanaotetea kutokana na elimu yao na wanasema kwa ujasiri mkubwa kwamba "kupiga punyeto ni sehemu ya maisha ya mwanadamu" Ina maana katika maisha ya mwanadamu upigaji punyeto inaelezwa ni kama tendo la lazima mpaka inafikia mahali wanasema ni sehemu ya maisha (Maisha) ya mwanadamu. Nimekuwa nikipata kesi nyingi sana juu ya madhara yatokanayo na punyeto. Aslimia 60