Skip to main content

FIGO NA VIHATARISHI 8 USIVYOFAHAMU VYA FIGO










1. NYAMA NYEKUNDU

Protini ni muhimu kwa afya zetu, lakini kama figo zako zina hitilafu, ama ulishawahi kupata vipimo na kujua kuwa figo zako haziwezi kuhimili vyakula vyenye protini nyingi sanasana ile protini itokananyo na nyama nyekundu basi unahitaji kupunguza matumizi makubwa ya nyama nyekundu na badala yake ukatumia vyakula vingine vyenye protini kama samaki, mayai, maharage, na karanga.

2.CHUMVI

Kwa  baadhi ya watu matumizi makubwa ya chunvi yanaweza kuongeza chembechembe za protini kwenye mkojo, hii inaashiria kwamba figo yako haiko vizuri kiafya na pia inaweza kuashiria kufanyika kwa mawe kwenye figo (kidney stones) ambayo yanaweza kuleta dalili kama maumivu makali pembeni mwa tumbo, na maumivu wakati wa kukojoa.

3. UVUTAJI WA SIGARA

Uvutaji wa sigara siyo tu unaongeza presha ya damu na kusababisha  kisukari ambayo ni magonjwa yanayoongoza kusababisha matatizo ya figo lakini pia uvutaji wa sigara hupunguza mzunguko wa damu kwenye figo nahivyo kuletekeza matatizo ya figo.

4. UNYWAJI WA POMBE

Matumizi makubwa ya pombe ni hatari kwa afya yako, wanaume wanaotumia zaidi ya chupa 14 kwa week na wanawake wanaotumia zaidia ya chupa 7 kwa week wapo katika hatari kubwa mara mbili ya kuugua magonjwa ya figo.

5. MATUMIZI YA SODA

Matumizi ya soda mbili kwa siku yanakuweka katika hatari kubwa ya kupata magonjwa ya figo.

6. UPUNGUFU WA MAJI

Figo zako zinahitaji maji safi kwa wingi ili kufanya kazi vizuri. Kutopata maji kwa wingi husababisha matatizo ya figo, unywaji wa maji vizuri husaidia kusafisha sumu na kupunguza hatari ya kuzeesha figo.

7. VIDONGE VYA KUPUNGUZA MAUMIVU

Matumizi ya mara kwa mara ya vidonge vya kupunguza maumivu mfano aspirini, ibuprofen huleta madhara kwenye figo zako. Ongea na tabibu wako kama kuna kuna njia ingine unaweza kutumia kupunguza maumivu  badala ya kumeza vidonge.

8. MADAWA YA KULEVYA

Matumizi ya cocaine, herion na madawa mengine ya kulevya huleta madhara na kupunguza utendaji kazi wa figo yako. Baadhi ya dawa hizi huongeza presha ya damu na kupelekea kutofanya kazi vizuri kwa figo.
Kama una maoni ama ushauri ama unahitaji tiba basi usisite

Kubofya hapa kuchati na Daktari kwa Whatsapp 


 utapata tiba na virutubisho kwa gharama ya sh 90,000/=   Kumbuka kushare pia na marafiki na ndugu

Usiache kufuatilia makala yetu inayofuata: Jinsi ya kujikinga na mawe kwenye figo pasipo kumeza vidonge. 

Comments

Popular posts from this blog

KUTOKWA NA UCHAFU UKENI, CHANZO NA TIBA YAKE

Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke. Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi. Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke. Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili. Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha. Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eno la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni. Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa. Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke. Uchafu Wa Sehemu Za Siri  Wa Kawaida Wanawake wote hutoa uchafu sehemu za siri. Kiwango cha uchafu unaotoka, ra

JINSI YA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATIZO YATOKANAYO NA KUKUA KWA TEZI DUME KWA KUTUMIA VYAKULA HIVI VI 5

Maelezo ya utangulizi. Kichocheo cha testosterone, japo huusishwa zaidi na upande wa mwananume ni muhimu kwa afya ya pande zote mbili yaani mwanamke na mwanamme pia.kadiri umri unavoenda mbele basi kiwango cha uzalishaji wa kichocheo cha testerone kupungua, kupungua kwa kichocheo hiki kunaambatana na ukuaji wa tezi dume (prostate gland),kupotea kwa nywele na pia saratani mfano saratani ya tezi dume. .KAZI KUBWA YA KICHOCHEO HIKI NI KUONGEZA MSUKUMO NA HAMU YA TENDO LA NDOA , KUIMARISHA MISULI NA MIFUPA MWILINI. NINI KINAHITAJIKA ILI KUZALISHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE? Ili kuhakikisha uzalishaji wa kichocheo cha kiume unafanyika, mwili unahitaji virutubisho au viini lishe mbalimbali, baadhi ya viini lishe hivyo ni madini ya ZINC na vitamin D3,  vitamini D inaweza kuzalishwa na mwili pale ngozi yako inapokutana na mwanga wa jua, hapa nazungumzia mwanga wa asubuhi wakati jua ndo linachomoza na pia lile jua la jion karibia na kuzama, hivyo utakubaliana na mimi kuwa wengi wet

MADHARA YA PUNYETO NA TIBA YAKE

MAELEZO  YA AWALI KUHUSU TATIZO LA UPIGAJI PUNYETO Watu wengi sana wanataka kufahamu jinsi gani wafanye ili kuachana na kitendo cha upigaji punyeto. Punyeto ni tendo la mtu la kuamsha hisia za mapenzi au msisimko ambao unampelekea mtu huyu kufikia kilele cha kujimalizia tamaa zake! Bila kufanya tendo halisi, hutumia fikra zake katika picha za zinazoitwa za ngono au picha zozote zinazoweza kulifanikisha tendo hilo, movie n.k. Kilele cha yote anafikia mahali anajimalzia tamaa zake mwenyewe!. Nimekuwa nikiona baadhi ya watu wanaosema wameelimika wakipingana wao kwa wao katika suala zima la kupiga punyeto! Wako wanaotetea kutokana na elimu yao na wanasema kwa ujasiri mkubwa kwamba "kupiga punyeto ni sehemu ya maisha ya mwanadamu" Ina maana katika maisha ya mwanadamu upigaji punyeto inaelezwa ni kama tendo la lazima mpaka inafikia mahali wanasema ni sehemu ya maisha (Maisha) ya mwanadamu. Nimekuwa nikipata kesi nyingi sana juu ya madhara yatokanayo na punyeto. Aslimia 60